SERIKALI MBIONI KUFUNGA ZIWA VICTORIA, TANGANYIKA WACHUHUZI WAFUNGUKA KUKIFUNGWA TUTA....
siku moja Ziwa Tanganyika lifunguliwe Agosti 15, 2024, Serikali imewataka wasimamizi wa Ziwa Victoria kuandaa mkakati wa kulifunga. Ziwa Tanganyika lilifungwa Mei 15, 2024, ili kutoa nafasi kwa ziwa hilo kupumzika na mazao ya uvuvi kuzaliana na kuongezeka ziwani. Akizungumza leo Jumanne Agosti 13, 2024, kwenye ufunguzi wa kongamano la Ukuzaji viumbe maji linalofanyika jijini Mwanza kwa siku tatu kuanzia leo mpaka Agosti 15, 2024, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexender Mnyeti amesema bila kufanya hivyo kuna uwezekano mkubwa miaka ijayo viumbe maji wakapotea. "Ziwa Victoria limetumika sana bila kupumzika, tuwaombe watu wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO), sisi huku hatuwezi kusema tufunge ziwa, hapana, ebu lianze kwenye ngazi husika mjadili kutoka ngazi za chini mpaka lifike huku juu, ili tufike mahala tufanye maamuzi ya kufunga hili ziwa kwa sababu tusipofanya hivyo ziwa hili linapoteza kila kitu," amesema Mnyeti. "Tumejaribu kupumzisha Ziwa Tanganyika kuanzia Mei 15 mpaka Agosti 15 ya kesho kutwa ambapo tunaenda kufungua. Tuliwatuma wataalamu wakaleta majibu kuwa mazalia ya samaki na dagaa yameongezeka kwa kiwango kikubwa katika Ziwa Tanganyika, kwa hiyo hili lichukuliwe kwa uzito mkubwa na sisi likija kwetu tutalibariki," ameongeza Mnyeti. Soma zaidi www.mwananchi.co.tz

YANATISHA:NILIYOYAONA ZIWA VICTORIA /MAAJABU YA JIWE/UCHAWI/NI ZAIDI YA MAAJABU/JIWE

HIZI HAPA HATUA ZA MAENDELEO YA MIRADI ZIWA VICTORIA

NOMA! ONA WANAUME WALIVYOSHINDANA KUENDESHA MITUMBWI ZIWA VICTORIA!

ONGEZEKO LA MAJI ZIWA VICTORIA LAVUNJA REKODI KUWAHI KUTOKEA KWA MIAKA 50

Kina cha maji chaongezeka Ziwa Victoria, nyumba zazingirwa maji

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

TAZAMA KIVUKO KIPYA MV. ILEMELA KINAVYOINGIZWA ZIWA VICTORIA!

Sababu Ziwa Victoria kufurika zabainishwa, tahadhari yatolewa

AJALI! MASHUA YAZAMA ZIWA VICTORIA, WATU 5 WAPOTEA HUKU WENGINE 6 WAKIOKOLEWA, UCHUNGUZI WAENDELEA..

Kivuko cha MV Nyerere chazama Ziwa Victoria (Ukerewe), takriban watu 40 wapoteza maisha

NILIMUOMBA KAKA ANILIPIE KODI YA MIEZI MITATU NIBAKI DAR | NIMETOKA KIJIJINI SANA | MAJID NSEKELA

Wavuvi 80 Wakwama Ziwa Victoria

Meli kubwa kuliko zote Ziwa Victoria kushushwa majini Februari 12

MAAJABU YA ZIWA VICTORIA: JIWE HILI/ USHIRIKINA WATAJWA/ "MWANAMALUNDI"/ MELI ZINAOGOPA

Ziwa Viktoria laingilia makazi ya binadamu baada ya kuvunja kingo zake

"BABA HAKUWA KWENYE HALI NZURI - PRESHA ILIKUWA JUU SANA" - MTOTO wa MZEE ONYANGO kwa UCHUNGU....

UJENZI MELI MPYA ZIWA VICTORIA WAFIKIA PATAMU

Hii ndio meli iliyoanza kazi Ziwa Victoria | Sifa zake na kasi yake majini

FAHAMU KUHUSU MAPATO YANAYOKUSANYWA NA BANDARI ZA ZIWA VICTORIA

