WIZARA YA ELIMU YAFANYA MAKUBWA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA (ATC)

KUTOKANA na kupatiwa vifaa vya kisasa na Serikali kupitia Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia,Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) kipo mbioni kutengeneza gari litakalotumia umeme. Hayo yameelezwa na Mkufunzi kutoka Idara ya Magari katika Chuo cha Ufundi Arusha,Mhandisi David Raymond wakati akizungumza na Waandishi wa Habari waliofika Chuoni hapo katika ziara ya kuangalia maboresho yaliyofanywa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia katika chuo hicho. Mhandisi huyo amesema maboresho yaliyofanywa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia yamewagusa kwa kiasi kikubwa kwani wameweza kupata vifaa vya kisasa na wanafunzi wanasoma kwa urahisi na wengi wamekuwa wakielewa kutokana na kusoma kwa vitendo