KIGOMA YAPATA KIWANDA CHA KUKAUSHA DAGAA, HASARA YA UVUVI KUPUNGUA KWA ASILIMIA 40.
Serikali mkoani Kigoma kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) imekamilisha ujenzi wa kiwanda cha kukausha dagaa na kutengeneza barafu kwa ajili ya kuhifadhi samaki, hatua inayotarajiwa kuokoa zaidi ya asilimia 40 ya mazao ya uvuvi yanayoharibika kila mwaka. Mradi huo unalenga kupunguza hasara kubwa iliyokuwa ikiwakumba wavuvi kutokana na ukosefu wa teknolojia za kisasa za kukausha na kuhifadhi samaki na dagaa, hasa kipindi cha mvua. Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi kiwanda hicho kwa serikali katika mwalo wa Katonga, Manispaa ya Kigoma Ujiji, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Mohammed Sheikh, akiwa pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma, Hassan Rungwa, wamesema kuwa mradi huo ni hatua muhimu katika kuimarisha sekta ya uvuvi na kuinua uchumi wa wavuvi. Wameeleza kuwa kupatikana kwa miundombinu hiyo kutasaidia kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kuboresha ubora wa samaki na dagaa pamoja na kufungua fursa za masoko ya ndani na nje ya nchi. Kwa upande wao, wachakataji wa dagaa na samaki mkoani humo wameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutekeleza mradi huo, wakisema utawasaidia kupunguza hasara na kuongeza kipato chao. Wameeleza kuwa awali walikuwa wakikumbwa na changamoto kubwa ya uhifadhi wa mazao yao, hali iliyosababisha baadhi ya samaki na dagaa kuharibika kabla ya kufika sokoni, lakini sasa matumaini yao yameongezeka kufuatia kukamilika kwa kiwanda hicho.

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

SIRO AWATAKA WATUMISHI KIGOMA KUZINGATIA NIDHAMU YA KAZI

Uzuri wa Kigoma - Mwisho wa Reli, @ Drone Footage - TANZANIA.

Wasira Kuhusu CCM Kujitathimini: Tulichepuka, Tunataka Kurudi Njia Kuu

Traoré’s Massive Irrigation Network Is Stunning the World

BABA LEVO APIGWA MASWALI NA WANANCHI WA KIGOMA"MIKATABA YA BUNGENI NI YA KINGEREZA NA HUJUI" ...

Shell and Chevron Abandoned This Coastline. Dangote Just Bought In.

TRUMP ATOA AHADI KWA DUNIA LEO HAIISHI ‘’MTAJUA NITAENDA KUIFANYA NINI IRAN’’ HAPA TUMEFIKA PABAYA

WAUMINI 700 TABORA, KIGOMA WAPATIWA MBINU ZA KUJITEGEMEA KIUCHUMI

WAZIRI MKUU ATAMKA RASMI KIGOMA KUPANDA HADHI, RAIS AMENIAMBIA NIWAAMBIE HILO, WATENDAJI KUBADIRIKA

MBUNGE DKT. MAHERA AITAKA SERIKALI KUONGEZA VYANZO VYA UPATIKANAJI WA UMEME.

Inside the Largest Wood Sawmill Factory – How Plywood Is Made From Logs to Table (Full Process)

When Tyson Faced the Smash Machine

SIFUNA SHOCKED AFTER RUTO RESPONDS TO HIM AT UTUMISHI ACADEMY REQUIEM MASS!!

DOGO ALIYETENGENEZA GARI LA UMEME KIGOMA, MASOUD KIPANYA AKUBALI UWEZO WAKE, NI SIKU YA SAYANSI

TAZAMA MUSUKUMA ALIVYOCHALAZA KISUKUMA MBELE YA RAIS MAGUFULI JIMBONI KWAKE

Gas from Africa - Europe’s search for new suppliers | DW Documentary

BEI YA UFUTA YAPAA SOKONI IGUNGA.

HISTORIC COMEBACK BY THE GREATEST JAPANESE GENERATION OF ALL TIME AGAINST ANCELOTTI’S BRAZIL

