Hotuba ya Rais Magufuli kisiwani Pemba, Zanzibar
Magufuli: Uchaguzi umeshakwisha na utakuja tena 2020, huo ndio ukweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Uchaguzi umekwisha mimi nikachaguliwa kuwa Rais na naitwa John Pome Magufuli na nimefunga Makufuli yote na funguo nimeshatupa. Nataka niseme Mhe Dk Shein, wewe ndie Rais na inawezekana umekuwa mpole kidogo, huo upole weka pembeni, unasapoti yangu yote, atakaekuchezea chezea niambie hata kwa kuninong'oneza. Tushirikiane kwa nguvu zote, wanaojaribu kuchezea amani yetu, mimi niliwahi kwenda Libya, mojawapo ya nchi za Afrika zilizokuwa na raha ni mojawapo. Pakajitokeza watu wachache kwa kuahidiwa ahadi za uongo, Libya leo siyo mahali panapokalika, watu wanamwaga damu kila siku, watu walichezea amani, hata amani inalevya. Rwanda wakati wa genocide walikufa watu wanaokaribia milioni moja, mmenichagua kuwa Rais wenu, nna wajibu wa kuwaeleza ukweli, wanaofanya chokochoko tunawajua wengine, wafatilieni wote wanaochomachoma washughulikiwe wote bila huruma. Mna bahati mna Rais mpole sana na hata sura yake nzuri tu na ni Rais alietoka Pemba, ni kitu gani kinatusumbua. Mimi nilifanya nae kazi nikiwa naibu waziri na waziri, ninamfajhamu Dk Shein, mpeni ushirikiano. Kuna mtu alijifungia kwenye chumba alafu akasema ametoka Ulaya, msikubali kudanganywa, hivi karibuni alinunua Meli na zinafanya kazi, kuna maeneo mengi yamepelekwa maji na umeme, watu hamtaki kuyaona haya. Palikuwa na Prof Mbarawa hapa mkamkataa jimbo la mkoani(Mkanyageni) mkamkanyagia hukohuko, mimi nnafahamu umuhimu wake na nikachukua wizara tatu nikaziunganisha zote nikampa mtu aliekanyagwa huku. Mpeni ushirikiano Dk Shein, imebaki miaka minne tu na kitu na kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar hiki ndio kipindi chake cha mwisho. Nawaomba wananchi tujenge umoja wetu. Tukienda kwa umoja wetu tutafanikiwa, tunataka tuimarishe uvuvi, mazao na serikali iliongeza hela kununua karafuu japo pato lake limeanza kushuka, tunataka tujenge hii nchi. Katika kipindi kifupi Pemba itakuwa kama Ulaya na wanaoharibu Pemba ni watu wachache sana. Wengine wanasema uchaguzi utarudiwa, kwa kawaida ndoto huwa ni usiku lakini hizo ni ndoto za usiku, lakini ukimkuta mtu anaota mchana, huyo anatafuta ukichaa. Nampongeza sana nh Jecha kwa kusimamia uchaguzi na umeenda vizruri sana na kama kuna tuzo mheshimiwa Shein utatoa, Jecha umpe hizo tuzo. Napongeza sana vyombo vya ulinzi, mmefanya kazi nzuri sana, mmesimamia amani ya Tanzania kwa uzalendo mkubwa sana.

Hotuba ya Rais Magufuli Unguja, Zanzibar

MAGUFULI: Msinichagulie shikamoo Zanzibar, nitapata shida...

HOTUBA YA RAIS MAGUFULI AKIWA UKEREWE - 04/09/2018

Tanzania yapiga marufuku mikutano ya kisiasa. Katika Dira ya Dunia TV

President, Julius Malema’s round table discussion on the Frank Dialogue

Unity Club Meeting | Opening Remarks by President Kagame | Kigali, 27 June 2026

Tujadiliane Tanzania na Zitto Kabwe

Perezida Kagame yavuze kuri Kayumba, Karegeya, Rudasingwa n’abandi | Ukuri kw’amateka no kwicuza

RAIS DKT MAGUFULI AKIZINDUA JENGO LA MAKAO MAKUU YA TARURA ENEO LA MJI WA SERIKALI - MTUMBA

"RPC UMLIPE HUYU MAMA MILIONI 15 - HUYO GADDAFI YUKO WAPI KWANI? - JPM...

MKUTANO WA RAIS MAGUFULI NA WAFANYABIASHARA

President Obama and President Kikwete Hold a Press Conference

RAIS MAGUFULI AFICHUA SIRI KUHUSU DK. HUSSEIN MWINYI "SIJWAHI KUWAPA HII SIRI"

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu

LIVE: UHURU KENYATTA AKIPOKELEWA CHATO NA RAIS MAGUFULI

Kipindi , ziara ya Rais Dkt Magufuli kisiwani Pemba,sept 02,2016

ALICHOKIFANYA RAIS MAGUFULI ZANZIBAR KAMWE HAKITOSAHAULIKA ,WATU WAMWAGA MACHOZI

From the archives: Barack Obama's 2004 DNC speech

Duh! ASKARI KIBURI Abishana na MAGUFULI Mbele ya RPC - "AMENIINUA"

