Chris B Gospel - Msamaha wa Kristo (Official Audio Music)

1. Waefeso 1:7 “Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.” 2. Wakolosai 1:13-14 “Naye alituokoa kutoka katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi.” 3. 1 Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” 4. Isaya 1:18 “Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji.” 5. Zaburi 103:12 “Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.” 6. Matendo 13:38 “Basi, na ijulikane kwenu, ndugu zangu, ya kuwa kwa huyo mnahubiriwa msamaha wa dhambi.” 7. Mathayo 26:28 “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.” 8. Warumi 5:8 “Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu tulipokuwa tungali wenye dhambi.” 9. Isaya 53:5 “Lakini alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu.” 10. Waebrania 8:12 “Kwa maana nitawasamehe maovu yao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena.” 11. Mika 7:18 “Ni nani aliye Mungu mfano wako, asameheye uovu?” 12. Luka 23:34 “Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui watendalo.” 13. Marko 11:25 “Msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu.” 14. Warumi 8:1 “Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” 15. Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee.” #tanzania #eastafrica #congo #gospel #church