HISTORIA NI HESHIMA YAKO (GILGALI) / REV. DR. ELIONA KIMARO
IBADA YA JUMAPILI TAREHE 15, JUNE 2025 KKKT KIJITONYAMA. KICHWA CHA SOMO: HISTORIA NI HESHIMA YAKO (GILGALI) Yoshua 4 : 17 Yoshua 4 : 19 - 24 Yoshua 4 : 17 17 Basi Yoshua akawaamuru hao makuhani, akawaambia, Haya, kweeni mtoke Yordani. Yoshua 4 : 19 - 24 19 Na hao watu wakakwea kutoka Yordani siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, wakapiga kambi Gilgali, katika mpaka wa mashariki wa Yeriko. 20 Na yale mawe kumi na mawili waliyoyatwaa katikati ya Yordani Yoshua akayasimamisha Gilgali. 21 Akawaambia wana wa Israeli, akasema, Watoto wenu watakapowauliza baba zao katika siku zijazo, wakisema, Mawe haya maana yake ni nini? 22 Ndipo mtakapowaarifu watoto wenu mkisema, Israeli walivuka mto huu wa Yordani, kwa njia ya nchi kavu. 23 Kwa sababu Bwana, Mungu wenu aliyakausha maji ya Yordani, mbele yenu, hata mlipokwisha kuvuka kama Bwana, Mungu wenu, alivyoitenda Bahari ya Shamu, aliyoikausha mbele yetu hata tulipokwisha kuvuka; 24 watu wote wa duniani wapate kujua mkono wa Bwana, ya kuwa ni mkono wenye uweza, ili wamche Bwana, Mungu wenu, milele. HOJA ZA KITHEOLOJIA NA FALSAFA. 1. HISTORIA NDIYO ILIYOBEBA HESHIMA YA MTU, IJAPOKUWA WATU WENGI HAWAPENDI HISTORIA YA MAISHA YAO 2. MPAKA SASA YESU HAJAONDOA HISTORIA YAKE DHAIFU YA UMASKINI WA KUZALIWA HORI LA NG'OMBE, MAISHA YA UMASKINI NA UKIMBIZI MISRI, FAMILIA MASKINI YA SEREMALA, KIFO CHA IBU MSALABANI NA KUFUFUKA SIKU YA TATU. KUZALIWA HORI LA NG'OMBE Luka 2:7 7 akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng'ombe, kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni. MAISHA YA UMASKINI NA UKIMBIZI MISRI Mathayo 2:13 13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize. 14 Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri; 15 akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu. FAMILIAMASKINI YA SEREMALA Marko 6:3 3 Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake. KIFO CHA AIBU MSALABANI NA KUFUFUKA SIKU YA TATU Yohana 19:17 17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha. Yohana 19:18 18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati. 3. KILA MTU ANA HISTORIA YAKE NGUMU INAYOMPA UMAARUFU NA HESHIMA....IBRAHIMU BABA WA IMANI ILA ALIZAA NA HOUSE GIRL. 4. YUSUFU ALIYEILISHA DUNIA MIAKA SABA ALIUZWA NA NDUGU ZAKE, ALIJARIBIWA KUBAKWA NA MKE WA POTIFA, ALIFUNGWA GEREZANI MIAKA MITATU NA BAADAYE KUWA WAZIRI MKUU WA MISRI KUUZWA NA NDUGU ZAKE Mwanzo 37:28 28 Wakapita wafanya biashara Wamidiani; basi wakamtoa Yusufu, wakampandisha kumtoa katika birika, wakamwuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande vya fedha ishirini; nao wakamchukua Yusufu mpaka Misri. KUBAKWA NA MKE WA POTIFA Mwanzo 39:11 11 Ikawa, siku moja, akaingia nyumbani atende kazi yake, wala hapakuwa na mtu katika watu wa nyumbani humo ndani; 12 huyo mwanamke akamshika nguo zake, akisema, Lala nami. Yusufu akaiacha nguo yake mkononi mwake, akakimbia, akatoka nje. ALIFUNGWA GEREZANI MIAKA MITATU Mwanzo 39:20 20 Bwana wake akamtwaa Yusufu, akamtia gerezani, mahali walipofungwa wafungwa wa mfalme, naye akawamo humo gerezani. KUWA WAZIRI MKUU WA MISRI Mwanzo 41:39 39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe. 40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe. 41 Farao akamwambia Yusufu, Tazama, nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri. 5. SARA ALIKUWA NA HISTORIA YA KUUZWA MARA MBILI AKIDANGANYA YEYE NI DADA WA IBRAHIMU KWA SABABU YA NJAA, ALIMTAFUTIA MUME WAKE MKE MWENZA, KISHA AKAMTESA SANA HAJIRI, ALIZAA BAADA YA KIKOMO CHA UZAZI, VILIMPA HESHIMA YA KUZAA TAIFA LA ISRAEL. Mhubiri: Rev. Dr. Eliona Kimaro.

MAISHA NI KUWEKEZA ( NYWESHA NGAMIA MAJI) : REV. DR. ELIONA KIMARO

MANASE & EFRAIMU / REV. DR. ELIONA KIMARO

KUKUA KATIKA KUMJUA MUNGU | Mwl.Mgisa Mtebe

This is my side of the story: Captain Patrick Waweru’s wife opens up | Tuko TV

Bwana Akubarikie na Kukulinda | Ibada ya Jpl, Kusifu na Kuabudu, 5 /2/ 2025 | Rev. Dr. Eliona Kimaro

KATIKA KRISTO KILA JARIBU LINA MLANGO WA KUTOKA

UJUMBE HUU NI WAKO | MUNGU ATAKUFURAHISHA | HAIJALISHI UNAPITIA NINI WAKATI HUU ~ Rev. Eliona Kimaro

🔴#LIVE: 15.07.2026 || HATUA TATU ZA KUPATA SEHEMU YA 1 || PR DAVID MMBAGA

WHEN BISHOP GWAJIMA WENT TO TEST HIS STRENGTH AGAINST A LOCAL HEALER

HUTATOKA KITUPU (THE POWER OF EMPTINESS) / REV. DR. ELIONA KIMARO

AFRICAN BILLIONAIRES AND THEIR WEALTH SECRETS ~ Dr. Eliona Kimaro | Do what they did (Part 2)

MATENDO YAKO YATAKUFUATA / REV. DR. ELIONA KIMARO

PEKE YAKO NA MUNGU (ALONE WITH GOD)/ REV. DR. ELIONA KIMARO

I have been out there working to ground my family, now I am living in isolation.

🔴LIVE | SEMINA YA KUTENGWA NA ROHO ZA MIZIMU | SIKU YA 2 | 30 MAY 2026

YAFAHAMU HAYA UHARAKISHE MAFANIKIO YAKO KATIKA UMRI ULIONAO ~ Dr. Eliona Kimaro

Kwa Ajili ya Haki / Because Of Righteousness / Rev. Dr. Eliona Kimaro

Ingeso nziza no Gukiranuka | Apostle Dr Paul M. GITWAZA | 22.7.2026

JINSI YA KUSHINDA ROHO YA KUKATA TAMAA

