"KUTOA NI MOYO INATOA FURSA KWA KILA MTANZANIA KUWA SEHEMU YA KUOKOA MAISHA". DR. NAIZIHIJWA MAJANI

Afisa Mtendaji Mkuu wa Heart Team Africa Foundation(HTAF), Dkt. Naizihijwa Majani, atoa wito kwa wadau na kila mtanzania kuchangia matibabu ya watoto wenye magonjwa ya moyo wasiokuwa na uwezo ili kujenga Taifa lenye ustawi. Amesema Taifa lenye Moyo wa kusaidiana hujenga kizazi chenye afya, nguvu na matumaini ya kesho.