AHADI zote za Mungu Zinasimama, Nyimbo za wokovu

163. AHADI zote za Mungu Zinasimama kweli, Na zilitiwa muhuri Kwa damu yake Yesu. Mbingu zikiondoka, Nchi ikitoweka, ’aminiye ’taona: Ahadi zinadumu. 2. Fanya kama Ibrahimu: Uangalie juu! Nyota ukizihesabu, Imani itaota. 3. Katika giza njiani Tutaamini tu. Muda kitambo, na tena Jua litaangaa. 4. Watu wakitusumbua, Tutaamini tu. Yesu atusaidia Majaribuni pote. 5. Kama rafiki wakosa, Tutaamini tu. Yesu, Rafiki mkubwa, Atabaki daima. 6. Katika mambo yo yote Tutaamini tu. Tutaviona mbinguni Tulivyoviamini. ”löftena kunna ej svika” Sgt. 254 (70), Evgt. 382, M.A. 14. Lewi Pethrus 1913