📌 WASIRA AFICHUA SIRI CCM KUJIFANYIA TATHMINI.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kutaka Chama kijifanyie tathmini, unalenga kupata viongozi bora na kushughulikia kikamilifu changamoto za Watanzania. Amesema wakati wana CCM wakielekea katika uchaguzi mkuu wa Chama, ni vyema kila mmoja kujitathmini kabla ya kuomba nafasi ya uongozi kuhakikisha ana sifa zikiwemo za kimaadili. Wasira aliyasema hayo jana mkoani Kigoma alipokuwa akizungumza na viongozi wa CCM kwa Nyakati tofauti katika wilayani Buhigwe, Kasulu pamoja na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Mkoa, akiwa katika ziara ya kichama mkoani humo. Alisisitiza viongozi na wanachama wa CCM kuijua na kuizingatia Katiba ya Chama, kanuni na miongozo inayoongoza uendeshaji wa Chama. “Siku hizi tunasema kuna njia kuu na mchepuko, njia kuu ya chama hiki imeandikwa katika hivi vitabu (Katiba, kanuni na miongozo) mchepuko ni tabia tunayoendesha nayo ambayo inapingana na vitabu, kwa hiyo tumechepuka tunataka kurudi njia kuu. Chama kinachoundwa na katiba hii kina madhumuni,malengo,Sifa za mwanachama, masharti ya kiongozi, wanachama, katiba na Kanuni. “sifa za uongozi, hizi zipo katika kitabu kinaitwa kanuni za uchaguzi ndani ya CCM, inasema sifa ya kwanza kiongozi wa Chama akinai maadili ya Chama kwa maana ya kwamba ayajue na ayaishi na asiwe mtu wa kuyumbayumba katika mambo ya msingi. “Unajua unaweza ukachagua kiongozi leo ana hili kesho ana lile sasa unaweza kumuuliza wewe hasa unasimamia nini maana yale uliyoyakubali jana ndiyo unayoyapinga kesho…wewe nawe ni mwanachama hatari na mwanachama wa namna ile anaweza akakidhulumu chama chenyewe. Makamu Mwenyekiti Wasira alisisitiza kiongozi anapaswa kuwa na uwezo wa kazi anayoiomba. “Kama wewe unataka kuwa mwenyekiti wa kata na hii inatuhusu baadhi kwa sababu mwaka kesho tuna uchaguzi, uombe kazi unayoiweza, uombe kazi na nafasi ya uongozi unayoiweza kwa wakati huo na usije ukasema unaziweza kwa wakati wote, hapana. “Tunataka viongozi wa chama hiki kwanza wawe wanachama kwa sababu viongozi wanatokana na wanachama, wanachama wanaoelewa watachagua viongozi wanaoelewa, wanachama ambao hawaelewi watarubuniwa na kumchagua ambaye haelewi kuliko wao, maana uongozi sio utajiri,” alisema. Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti Wasira, Halmashauri Kuu ya Taifa ilikutana jijini Dodoma hivi karibuni na kuazimia Chama kufanya tathmini ili kujiboresha. “Halmashauri Kuu ya Taifa imekutana juzi juizi Dodoma, tumekubaliana kwamba tujitathmini, tukitathmini chama chetu na tathmini isitoke juu, itoke kwa wanachama kwenye matawi yao, kwenye kata zao mtuambie hiki chama kama tumekosea, tumekosea wapi tusahihishe nini ili tuweze kusonga mbele. “Haya si mambo yangu, ni uamuzi wa halmashauri kuu ya taifa tusahihishe, tujisahihishe tujitathmini maana sisi ni Chama cha wanadamu tunaweza kufanya makosa, lakini makosa ni makosa yanaweza yakasahihishwa. Hata ukiwa muumini wa dini yako ukaanguka unaweza ukarudi wakakubatiza upya, huko ni kujisahihisha,” alieleza. Katika hatua nyingine, Wasira aliwasihi wananchi kutohadaika wala kuvisikiliza vyama vinavyotumika kutaka kurudisha ukoloni. Alisema vipo baadhi ya vyama vya siasa ambavyo kwa matukio vinaonekana kubeba ajenda za watu walioko nje ya Tanzania kwa maslahi yao. “Kimekuja Chama hapa kinawaambia sisi tunataka kuchukua nchi, lakini chama hiki kinatumwa na wazungu, wazungu wako nyuma, wazungu wale wanajua ukoloni kurudi kabisa na bunduki ni ngumu, lakini wakikamata viongozi wenu au vibaraka waliowaweka wao wanaweza kuendesha nchi hizi wakanyonya rasilimali za taifa,” alisema.

EXCLUSIVE NA MSIGWA | MTOTO WANGU ALIONA ZILE MAITI OKTOBA 29 | AKANIULIZA KAMA NINGEUWAWA MIMI BABA
▶︎

EXCLUSIVE NA MSIGWA | MTOTO WANGU ALIONA ZILE MAITI OKTOBA 29 | AKANIULIZA KAMA NINGEUWAWA MIMI BABA

MH! MBUNGE SHABIBY ACHAFUA HALI YA HEWA, SHERIA YA KUNYONGA WATU 2030 'SITAKI LAWAMA KABISA'.....
▶︎

MH! MBUNGE SHABIBY ACHAFUA HALI YA HEWA, SHERIA YA KUNYONGA WATU 2030 'SITAKI LAWAMA KABISA'.....

Juma Lokole afunguka Diamond kumfukuza Diva kazi Wasafi Media| Hakuna anayemtaka| Hasara kubwa sana
▶︎

Juma Lokole afunguka Diamond kumfukuza Diva kazi Wasafi Media| Hakuna anayemtaka| Hasara kubwa sana

Lema Atoboa Siri Nzito Kuhusu Kauli ya Mwigulu Nchemba, Utekaji ni Michezo: 'Hakuna Anayekuogopa'
▶︎

Lema Atoboa Siri Nzito Kuhusu Kauli ya Mwigulu Nchemba, Utekaji ni Michezo: 'Hakuna Anayekuogopa'

MWANZO MWISHO MSAIDIZI WA LISSU ASIMULIA,ALIVYOTEKWA HADI KUTOROKA KUPIGWA NA BUNDUKI,KUIBIWA LAKI 7
▶︎

MWANZO MWISHO MSAIDIZI WA LISSU ASIMULIA,ALIVYOTEKWA HADI KUTOROKA KUPIGWA NA BUNDUKI,KUIBIWA LAKI 7

IJUE HISTORIA YA CHAMA CHA MAPINDUZI (ADAM PAULO NGALAWA ) KATIBU WA CCM MKOA WA MWANZA.
▶︎

IJUE HISTORIA YA CHAMA CHA MAPINDUZI (ADAM PAULO NGALAWA ) KATIBU WA CCM MKOA WA MWANZA.

EDO, OSCAR WAMLIPUA KIONGOZI CCM ALIYESEMA ''UKIWA CCM UNAENDA MBINGUNI''
▶︎

EDO, OSCAR WAMLIPUA KIONGOZI CCM ALIYESEMA ''UKIWA CCM UNAENDA MBINGUNI''

AMVUNJA MBAVU WAZIRI MKUU BAADA YA KUMWAMBIA KUWA ANAM SUPPORT YOUTUBE
▶︎

AMVUNJA MBAVU WAZIRI MKUU BAADA YA KUMWAMBIA KUWA ANAM SUPPORT YOUTUBE

Mwanzo-Mwisho Wabunge CCM Wachachamaa Marekani Kutaka Kuwaekea Vikwazo Viongozi wa Serikali Tanzania
▶︎

Mwanzo-Mwisho Wabunge CCM Wachachamaa Marekani Kutaka Kuwaekea Vikwazo Viongozi wa Serikali Tanzania

🔴#LIVE: MSAJILI KUIKALIA KOONI CCM? / CHADEMA WAMJIBU kwa VIFUNGU /NINI KINAENDELEA VYAMA vya SIASA?
▶︎

🔴#LIVE: MSAJILI KUIKALIA KOONI CCM? / CHADEMA WAMJIBU kwa VIFUNGU /NINI KINAENDELEA VYAMA vya SIASA?

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu
▶︎

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu

MBUNGE WA KATAVI AVUNA PESA ZA KUTOSHA BUNGENI BAADA YA KUPINGA VIKALI TABIA ZA KISHOGA
▶︎

MBUNGE WA KATAVI AVUNA PESA ZA KUTOSHA BUNGENI BAADA YA KUPINGA VIKALI TABIA ZA KISHOGA

KAULI YA WASIRA YAIBUA MASWALI, WAHUSIKA VURUGU OKTOBA 29 WAPATIKANE!
▶︎

KAULI YA WASIRA YAIBUA MASWALI, WAHUSIKA VURUGU OKTOBA 29 WAPATIKANE!

🔴#live; EXCLUSIVE INTERVIEW YA TUNDU LISSU USIKU HUU AKIWA NA ODEMBA AFUNGUKA KILA KITU
▶︎

🔴#live; EXCLUSIVE INTERVIEW YA TUNDU LISSU USIKU HUU AKIWA NA ODEMBA AFUNGUKA KILA KITU

JE MAFWELE ATAKOSA KITU GANI BAADA YA KUWEKEWA VIKWAZO? | UCHAMBUZI
▶︎

JE MAFWELE ATAKOSA KITU GANI BAADA YA KUWEKEWA VIKWAZO? | UCHAMBUZI

Wasira Kuhusu CCM Kujitathimini: Tulichepuka, Tunataka Kurudi Njia Kuu
▶︎

Wasira Kuhusu CCM Kujitathimini: Tulichepuka, Tunataka Kurudi Njia Kuu

MBUNGE WA KATAVI AVUNA PESA BUNGENI BAADA YA KUGONGA NONDO ZITO JUU YA UVUNJIFU WA MAADILI.
▶︎

MBUNGE WA KATAVI AVUNA PESA BUNGENI BAADA YA KUGONGA NONDO ZITO JUU YA UVUNJIFU WA MAADILI.

Chris Rwakasisi Moves Ruto and Kenyans to Tears as he Narrates how Museveni Jailed him for 24 Years!
▶︎

Chris Rwakasisi Moves Ruto and Kenyans to Tears as he Narrates how Museveni Jailed him for 24 Years!

Iran, U.S. trade strikes overnight as war appears to reignite
▶︎

Iran, U.S. trade strikes overnight as war appears to reignite

🔴#LIVE: CHADEMA WANAUNGURUMA MUDA HUU KAHAMA MAELFU WAFURIKA KWENYE MKUTANO
▶︎

🔴#LIVE: CHADEMA WANAUNGURUMA MUDA HUU KAHAMA MAELFU WAFURIKA KWENYE MKUTANO