HELLO WIKIENDI | Lugha ya ukali haimjengi mtoto

Mlezi wa Makao ya Watoto ya Maunga Orphanage, Alexander Matowo, amesema malezi bora ya mtoto yanahitaji hekima, uvumilivu na ubunifu kutoka kwa wazazi na walezi, hususan baba. Matowo amesema matumizi ya lugha ya ukali yanaweza kuathiri ukuaji wa mtoto kisaikolojia na kijamii, hivyo amewataka wazazi kutumia lugha ya upole katika malezi. Ameeleza kuwa lugha ya upole na yenye kuelekeza humsaidia mtoto kujenga kujiamini, kujitambua na kuwa huru kueleza hisia na mawazo yake. Matowo ametoa kauli hiyo katika kipindi cha Hello Wikindi kilichoangazia umuhimu wa nafasi ya baba katika malezi ya mtoto, sambamba na maadhimisho ya Siku ya Baba Duniani.