UFUGAJI BORA WA NG'OMBE WA NYAMA

SIFA ZA DUME BORA LA NG'OMBE WA NYAMA KWA UZALISHAJI. Mafanikio ya ufugaji wa ng’ombe uanzia na uchaguzi mzuri wa dume kwa lengo moja tu kupata ndama ambaye atakuwa na matokeo mazuri ya ufugaji wa Ng’ombe wenye mafanikio. Kwa mfugaji wa ng’ombe wa muda mrefu au umekuwa ukitamani kuwa mfugaji wa ng’ombe kwa mara ya kwanza pia umekuwa una uzalishaji mdogo katika ufugaji wako kwa sababu mbali mbali kama tatizo ni dume bora la ng’ombe hizi hapa ni sifa bora kabisa za kuzingatia katika uchaguzi wa dume la ng’ombe kwa uzalishaji na kupata matokeo mazuri ya nyama. Upatikanaji wa dume la ng’ombe upo wa aina mbalimbali ikiwemo kwa kununua kutoka kwa kituo maalumu cha uzalishaji wa madume, au umekuwa na madume mengi na unataka kufanya chaguzi ya dume bora ambalo litaweza kuwa na uzalishaji wenye mafanikio sana, au pengine kuna mfugaji ambaye ana madume mazuri na unataka mbegu kwaajili ya zizi lako. Sifa za Dume. Sifa ya kwanza kabisa angalia ukoo anaotoka ng’ombe huyo, iwe ni koo ambayo haina historia ya utasa, magonjwa ya kuambukizwa kama magonjwa ya kuvimba viungo vya uzazi. Asiwe na ulemavu ikiwemo, ulemavu wa miguu au upofu. Awe na hamu ya kupanda. Awe mwenye afya bora. Awe mwenye nguvu kukabiliana na majike makubwa pamoja na madume mengine yenye ukubwa kama wa dume la uzalishaji. Dume achaguliwe akiwa na umri wa kuanzia miezi 9 na kuendelea Kagua sehemu zake za uzazi kama korodani kuhakisha kama hakuna dalili zozote za magonjwa kama kuvimba, au kama zimeungana. Muoekano wa korodani ni kiashilia kama dume huyo amekwisha pevuka na anauwezo wa kuzalisha mbegu bora. Pia korodani zinatakiwa kuwa zinazo onekana kwa urahisi (zilizo ning’inia wastani), ukipima ukubwa wa korodani uwe na Sentimeta 35. Muonekano Wa Viungo Vya Wa Dume. Awe na Macho yenye uwezo wa kuona vizuri. Awe na Taya zenye ukubwa wa wastani zitakazo muwezesha kula chakula vizuri. Shingo inatakiwa kuwa yenye urefu wa wastani Mabega yawe yenye kunyooka na sio yaliyo pinda, hali ya mabega kuwa yaliyo nyooka itamuwezesha kuwa mwepesi wakati wa kupanda. Miguu iwe yenye stamina na kwato zilizizo nyooka vizuri (kwa wastani) na sio miguu yenye matege. Muonekano wa kiungo cha kiungo cha uzazi (uume) uwe umejishikiza vizuri. chakula cha kunenepesha ng'ombe wa nyama bei ya ng'ombe wa nyama 2022 biashara ya kunenepesha ng'ombe dawa ya kunenepesha mifugo chakula cha ng'ombe wa maziwa pdf bei ya mbuzi vingunguti 2022 bei ya mbuzi dar es salaam 2022 bei ya ng'ombe wa nyama 2022 ufugaji wa ng'ombe wa kienyeji pdf biashara ya kunenepesha ng'ombe ufugaji wa ng'ombe wa maziwa tanzania ufugaji wa ng'ombe wa maziwa faida ya ufugaji wa ng ombe #mkulimasmart #shambadarasa