MOTO NCHIMBI: VIJANA NI NGUZO YA SEKTA YA AFYA YA KESHO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema unapotafakariwa mustakabali wa utoaji huduma za afya nchini, hakuna budi kutoa kipaumbele kwa vijana kama Hayati Benjamini Mkapa alivyoamini, ikiwemo kubuni programu zitakazowaandaa vijana kukabiliana na changamoto za siku zijazo kwa kujiamini. Makamu wa Rais amesema hayo, wakati alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Nne wa kuenzi na kuendeleza Urithi wa Hayati Benjamin William Mkapa na Maadhimisho ya Miaka 20 ya Taasisi ya Benjamin Mkapa (BMF), uliyofanyika katika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Amesema Vijana ndiyo viongozi wa sekta ya afya wa kesho, watumishi wa afya na watafiti wajao. Makamu wa Rais amesema Maisha na uongozi wa Hayati Benjamin Mkapa unatoa mafunzo mengi hususani katika usimamizi na uendelezaji wa sekta ya afya nchini kwa kuwa alitambua nafasi ya afya bora katika maendeleo. Ameongeza kwamba, Hayati Benjamin Mkapa katika awamu yake aliweka mkazo katika mapambano dhidi ya UKIMWI, Malaria na magonjwa mengine yanayoambukizwa na yasiyo ya kuambukiza. Amesema katika uhai wake, Hayati Mkapa aliamini katika kujenga taasisi na alitumia muda wake, nguvu na jitihada zake nyingi kuhakikisha taasisi hizo zinaimarika. Amesema ushahidi upo unaoonesha kuwa taasisi nyingi zilizoasisiwa katika uongozi wake bado zinaendelea kutekeleza majukumu yake ipasavyo. Makamu wa Rais amesema ni muhimu kiongozi katika sekta ya afya kuelewa uhusiano uliopo kati ya afya na uchumi, siasa, utamaduni, pamoja na muunganiko kati ya mifumo ya afya ya kitaifa na ya kimataifa. Ameipongeza Taasisi ya Benjamin Mkapa kwa kutoa mchango wake kwa sehemu kubwa kuwezesha viongozi katika sekta ya afya. Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema, viongozi wa awamu nyingine akiwemo Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, wameendeleza jitihada za kuimarisha sekta ya afya na kupambana na changamoto zake ikiwemo kusimama kidete kuongoza mapambano dhidi ya UVIKO-19 na magonjwa mengine. Amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika kukuza elimu ya sayansi, hususan katika taasisi za elimu ya juu kupitia programu mbalimbali. Makamu wa Rais amepongeza ushirikiano kati ya Taasisi ya Benjamin Mkapa na Wizara ya Afya katika kuanzisha jukwaa la vijana kujadili ajenda ya rasilimali watu katika sekta ya afya. Makamu wa Rais amewahimiza vijana kutumia kikamilifu fursa zitokanazo na maendeleo ya teknolojia kama akili unde, tiba kwa njia ya mtandao ,uchambuzi wa takwimu na teknolojia mpya zitakazoendelea kubadilisha tasnia ya afya. Makamu wa Rais ameunga mkono azma ya kuubadilisha Mkutano huo kutoka mkusanyiko wa mara moja kila baada ya miaka miwili, na kuwa jukwaa kuu la Afrika la fikra za kitaalamu, majadiliano ya sera, ubunifu na kubadilishana maarifa kuhusu nguvu kazi ya afya, litakalofanyika mara moja kila mwaka. Mkutano huo, umehudhuriwa na Mlezi wa Taasisi ya Benjamin Mkapa ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Viongozi mbalimbali wa Serikali, wadau wa maendeleo wa Kitaifa na Kimataifa, wadau wa sekta ya afya pamoja na wananchi.

Wadau Wajadili Onyo Kwa Wanaharakati: 'Taifa Limejengwa na Wanaharakati'

Air Tanzania Cockpit Boeing 767-300 Freighter to Kinshasa

Aliko Dangote’s $46B Warning to Africa: Industrialize or Remain Left Behind!

🚨 MTANZANIA PEKEE KWENYE MAZISHI YA KHAMENEI | AFICHUA AMEZIKWA NA WATU MILIONI 42 IRAN YOTE

Incredible Metal Magazine Manufacturing in Local Factory

PLO Lumumba: Why Iran Is Winning the War Against Israel & the USA | Oil, China & Dollar Explained

🔴🅻🅸🆅🅴 HakiTv : Katambi afunguliwa kesi Rasmi LHRC,TLS na Dkt. Slaa Wanafunguka

SAKATA LA POLEPOLE NA WENGINE WALIOTEKWA, WAZIRI KATAMBI AFUNGUKA "SERIKALI HAITEKI INAKAMATA"

NI VIGUMU SANA KUPATA DEGREE CHUO KIKUU CHA SUA | TUNAPAMBANA NA RUSHWA YA NGONO | PROF. CHIBUNDA

🔴#LIVE: MJADALA MZITO WA DEMOKRASIA,BAGONZA SHEIKH PONDA WANAUNGURUMA MUDA HUU

Body recovered from San Francisco Bay boat accident identified as Sacramento County woman

Samia vs The West: The REAL POWER PLAY Behind Tanzania's Protest

Trump Has "Really Big News" on Election Security

Russia Just Made EUROPE'S WORST NIGHTMARE Come True in Mozambique

"OTHMAN MASOUD AFUNGUKA MAZITO: 'MARIDHIANO SI YA ACT WALA CCM, NI YA WAZANZIBARI WOTE'"

#OTHMAN MASOUD AENDELEA KUPANGUA HOJA ZA UKOSOAJI MARIDHIANO NA CCM

BOT na TRA Waingilia Kati Mabilioni ya Harusi Katoro

RAIS SAMIA AWAJIBU JUMUIYA YA MADOLA SAKATA LA LISSU, "MATAMKO YANATUWEKA KATIKA WAKATI MGUMU"

Ministre ALAIN avuze Umugambi wo kwubaka umuji wa GITEGA//ivyitwazo vya REGIDESO kukibazo c'Amazi

#LIVE: WAZIRI KATAMBI AFUNGULIWA KESI NZITO SAKATA LA KUFUNGIA MIKUTANO YA HADHARA, MOTO WAWAKA

Sio mwanamke! Huu ndio ukweli kuhusu kuondolewa kwa Sheikh Alwalid katika nafasi ya Sheikh wa Mkoa.

🔴 #LIVE: ADVOCATE MADELEKA ANALYZES STATEMENTS BY PRESIDENT SAMIA AND THE CHIEF JUSTICE

Hegseth Announces Testosterone Tests & Vance Fixates on Biden’s Ice Cream Licking | The Daily Show

Trump's primetime speech: 'exaggerated claims' and 'conspiracy theories'

Could Xi's Vision for AI Clash With Trump's? | Insight with Haslinda Amin 7/17/2026

Mohammad Marandi: Iran Rejects US Demands as the Strait of Hormuz Crisis Explodes

John Mearsheimer & Yanis Varoufakis: Why America Keeps Losing Wars—Will Iran Be Different?

