WAZIRI MAKONDA WACHAWI NI WENGI MENGI KWENYE HII NCHI WANATABIA YA KUNENA VITU VISITOKEE

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amekuwa mgeni rasmi katika sherehe za kuadhimisha miaka 25 ya ushirikiano kati ya China na Urusi zilizofanyika Jijini Dar es Salaam. Sherehe hizo zilihusisha maonesho ya filamu ya pamoja ya China na Urusi ijulikanayo kama Red Silk, ikiwa ni sehemu ya kuenzi urafiki na ushirikiano wa muda mrefu kati ya mataifa hayo mawili. Akizungumza katika hafla hiyo, Makonda amepongeza ushirikiano wa China na Urusi, akisema Tanzania itaendelea kuimarisha mahusiano na nchi hizo katika sekta mbalimbali ikiwemo habari, utamaduni, sanaa na michezo. Hafla hiyo iliandaliwa na Ubalozi wa China na Ubalozi wa Urusi nchini Tanzania, ikiwakutanisha viongozi wa serikali, wadau wa sanaa na maafisa wa sekta ya filamu kwa lengo la kuendeleza urafiki na ushirikiano kati ya mataifa hayo na Tanzania.