OPARESHENI YA TRA SINGIDA WAFANYABIASHARA WAHIMIZWA KULIPA KODI KWA HIARI

SINGIDA Mamlaka ya mapato Tanzania TRA Mkoa wa Singida wamepita katika madaka mbalimbali wakihimiza suala la kulipa kodi pamoja na kusikiliza na kutatua changamoto za wafanyabiashara biasha hao katika maeneo yao ya Kazi. Akizungumza mara baada ya kutembelea wafanyabiashara hao meneja wa TRA Mkoa wa Singida Josephat Mwaipaja amesema mwezi huu ni nimwezi wa kulipa kodi awamu ya pili hivyo wamepitia kuwakumbusha wafanyabiashara kulipa kodi zao kwa wakati. Amesema katika ziara yao wamesikiliza na kutatua papokwa papo changamoto mbalimbali ambazo zilikuwa zikiwakabili wafanyabiashara hao. Katika hatua nyingine Meneja Mwaipaja amewashukuru walipa kodi kwa kuendelea kuufanya mkoa wa Singida kuvuka malengo katika suala la ukusanyaji wa Mapato. Amesema lengo la mwaka ni kukusanya bilion 30.54 ambapo kwa miezi kumi na moja walitakiwa kukusanya shilingi bilioni 27.23 lakini mpaka sasa wamekusanya shilingi bilioni 29.79 ikiwa ni ufanisi wa asilimia 109. Kwaupande wao baadhi ya wafanyabiashara wamepongeza mamlaka ya mapato TRA kwa kuendelea kuwatembelea na kutoa elimu ya mara kwa mara suala lililosaidia kuondoa changamoto #milardayo #rickmedia #bbc