Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460 Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa. Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM. Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya. Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu. Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu. Love, Salama. Support us through https://anchor.fm/yahstonetown/support SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs Listen our Podcast on Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One The Incredible & Msam... Follow: Twitter: / yahstonetown Instagram: / yahstonetown Facebook: / yahstonetown Channel Administered by Slide Digital Instagram: www.instagram.com/slidedigitaltz

Salama Na LULU DIVA SE6 EP61 | UKIPATA KINYAKUE… PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Salama Na MAJIZZO SE6 EP17 | MPIMAJI PART 1| SendTip MPESA LIPA NO 5578460

“MY WIFE TOLD ME I’M NOT THE BIOLOGICAL FATHER OF OUR FOUR CHILDREN” MR LATEEF

MASOUD KIPANYA ASIMULIA KATUNI YA MAGUFULI ALIYOICHORA ILIVYOTAKA KUMLETEA SHIDA/NILIPIGIWA SIMU

Salama Na KALITO Ep 41 | THE ORIGINATOR Part 1

ONE THE INCREDIBLE AFUNGUKA UKWELI MSIOUJUA KUHUSU NIKKI MBISHI |FID Q AMENIFANYIA MAMBO MENGI

Safari Ya Adam Mchomvu, Kusoma Uganda Mpaka Kufanya Kazi Clouds | SALAMA NA ADAM MCHOMVU PART 1

🔴#LIVE: MAPYA KESI ya LISSU KUPIGWA KALENDA /TAMU - CHUNGU BAJETI KUU LEO/WAZIRI AKANUSHA KAULI YAKE

Mkasi - S01E03 Masoud Kipanya

Gidi Na Ghost Asubuhi LIVE - Africa's Biggest Swahili Breakfast Show

Mkasi - SO7E06 With Masoud

Scars from Russia: Former KDF pilot narrates his escape from Russia war, going for days without food

"Nilianza Kujitegemea Nikiwa Na Miaka 17" AY Afunguka Maisha Kabla Ya Umaarufu | SALAMA NA AY PT 1

Salama Na Profesa ep 55 | MAPINDUZI HALISI Part 1

MASOUD KIPANYA: NDOTO ZINAKUFA/ "TUNAHITAJI SAUTI YA PAMOJA"/ WENYE VIWANDA/ WAZALISHAJI

Gerald Asimulia Siku Yake Ya 1 Redioni "Sikuamini Nilifikiri Ruge Ananitania" SALAMA NA GERALD PT 2

PART 1: PROF ASSAD AONGEA KWA UCHUNGU, WANAGOMBEA NA HAWAJUI CHAKUFANYA, SALIM KIKEKE KWA MAKINI

BREAKING! SAMIA KUMNG'OA NCHIMBI PUNDE | HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA MAKAMU KUWASILISHWA BUNGENI

LIVE: KASRI LA KIKEKE LIVE NA MASOUD KIPANYA NA MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO NIDA

