MAUMIVU YA JICHO/MACHO: Kujitibu mwenyewe nyumbani
DR. MNIKO #MNIKO #DRMNIKO Maumivu kwenye jicho ni dalili muhimu na huwa sio rahisi kuipuuzia kwa muda mrefu. Ila kwa bahati nzuri, si jambo linalowapata watu wengi. Watu wengi huwa wanalamamika kuwashwa au kuhisi kama macho yanawaka moto. Maumivu ya jicho yanaweza kutokana na jerha, maambukzi au ugonjwa mwingine wowote mwilini. Moja ya ugonjwa muhimu unaoweza kusababisha maumivu kwenye jicho ni ugonjwa wa presha ya jicho (glaucoma). Ugonjwa wa presha ya jicho au glaukoma unaweza kusababisha mtu akawa kipofu taratibu kama hatapata matibabu. Kwa mgoonjwa mwenye ugonjwa wa glaukoma, majimaji yaliyomo ndani ya jicho yanakuwa na presha kubwa sana ambayo inaanza kuharibu jicho na kusababisha karha. Mara nyingi mtu mwenye tatizo hili, ataanza kuanza kushindwa kuona vitu kupitia kwenye pembe za macho kwanza. Taratibu ataanza kuona uwezo wake wa kuona unapungua kuanzia pembeni kwenda ndani mpaka atakuwa anaona kama yuko ndani ya tanuru Fulani “tunnel vision”. Mtu mwenye ugonjwa huu akiangalia taa inayotoa mwanga, mwanga utakuwa unamuuza sana (kama vile ukiangalia lile jua la mchana ukalikazia macho, ukitoa macho, unaona mzunguko mizunguko myeupe na kujisikia vibaya. Kwa bahati mbaya, dalili hizi zinaweza bado kuwepo, hata kama hauna maumivu ya jicho. Nikukumbushe kwamba maumivu ya jicho ni dalili ambayo inasababishwa na mambo mengi, na mara nyingi itahitajika kujua sababu yake ili kuitibu vizuri. Kuhidi macho yamechoka baada ya kufany kazi kwa muda mrefu ni tatizo dogo tu na mara nyingi huwezi kusema ni maumivu ya macho. Unaweza kuwa na maumivu makali ya jicho kwa sababu ya kipandauso au maumivu yaliyo juu au chini ya jicho yanaweza kuashiria maambukizi kwenye mianzi ya pua (sinusitis) Maumivu kwenye macho yote, hasa baada ya kuangalia mwanga “photophobia” ni kawaida kwa wagonjwa wengi wa mafua na yataisha baada ya mafua kupona. Kama unashindwa kuangalia mwanga au macho yanatoa machozi ukiangalia mwamnga, hasa inapokuwa kwney jicho moja pekee, inaweza kuashiria kuwa shemu ya ndani ya jicho imevimba – kwa hali kama hii unahitaji kuonana na daktari. Mambo ya kufanya ukiwa nyumbani kama una maumivu ya jicho Isipokuwa kwa maumivu ya jicho yanayoambatana na mafua au kuchoka kwa macho au karaha kiasi inayotokana na uchovu, hatushauri ujitibu ukiwa nyumbani. Kwa hali nyingine zote za macho kuuma nenda kaonane na daktari. Ila kama ni kwa hli hizo nilizotaja hapo juu, kupumzisha macho ndio tiba bora ziadi, tumia dawa ya acetaminophena na epuka kuangalia mwanga mkali. Kama maumivu yameendelea kuwepo kwa zaidi ya masaa 48 nenda kaonane na daktari.

#HABARI:FAHAMU KABLA HUJANUNUA MIWANI YA KUZUIA MIONZI YA JUA NA UREMBO | KAROTI NI TIBA YA MACHO

Tatizo la makengeza.

KINACHOSABABISHA PRESHA YA MACHO / SABABU YA UPOFU / USIPUUZIE

MEDICOUNTER: Fahamu chanzo, dalili na matibabu ya mtoto wa jicho

HOJA MEZANI | Chanzo cha matatizo ya macho na tiba ya miwani

MEDICOUNTER: Tatizo la UONI HAFIFU. Nini chanzo? Likoje? Na linatibikaje?

FAHAMU KUHUSU TATIZO LA KUSHINDWA KUONA MBALI

Glaucoma au presha ya macho

NIBA WIYITAHO MU MIRIRE NI ITEGEKO KUMENYA IBI BINTU 8. Ukabona byose umubiri wawe ukeneye.

What is Blepharitis and How to Cure it .... For Good.

Stop Treating Dry Eye Wrong | The Eyelid Connection

Dry Eyes That Won’t Go Away? THIS Finally Fixed It — Here’s Why Nothing Else Worked | Dr. Mandell

MTOTO WA JICHO (Ukungu jichoni): Sababu, Dalili, Matibabu

I SHOW 3 EXERCISES FOR CATARACTS

One Move to Clear a Stuffy Nose and Drain Your Sinuses | Dr. Mandell

KIUNGULIA: Sababu, Dalili, Matibabu, Kuzuia

KUWASHWA AU MACHO KUWAKA MOTO NA KUTOA MAJIMAJI/UCHAFU: Kujitibu mwenyewe nyumbani

Seniors: Eat THESE 3 Foods Before Bed to Repair Your Eyes & Restore Vision While You Sleep!

Mazoezi bora kwa maumivu ya shingo | Best Exercises for Neck pain in Swahili Kenya

