UPANUZI WA BARABARA YA NJIA NNE BUKOBA MJINI SERIKALI KUONGEZA BILIONI 4, KUKAMILISHA
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa tayari Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kuongeza kiasi cha Shilingi Bilioni 4 kukamilisha upanuzi wa barabara ya njia nne Bukoba Mjini (Rwamishenye Round about - Stendi ya Bukoba Mjini) yenye urefu kilometa 1.6. Bashungwa amesema hayo leo tarehe 28 Machi 2024 wakati alipowasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera kuanza ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya barabara Mkoani humo. Bashungwa amesema kuwa awali Serikali ilitoa kiasi cha shilingi Bilioni 4.64 kuanza ujenzi wa wa barabara hiyo kwa kipande cha kilometa 1 ambacho kinaanzia Rwamishenye hadi eneo la Mitaga ambapo kwa sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 25. Amesema kuwa kiasi cha shilingi Bilioni 4 kitakachoongezwa kitawezesha ujenzi wa kipande cha mita 600 kuanzia eneo la Mitaga hadi stendi na ujenzi wa daraja kubwa katika mto Kanoni. “Mheshimiwa Rais ameshatoa kibali kwa TANROADS kuendeleza ujenzi wa barabara ya njia nne hadi stendi ya Bukoba ambapo Mkandarasi M/s Abemulo ambaye ameshaanza kazi kwa kipande cha km 1 ataendelea na ujenzi kwa kipande cha mita 600 na daraja kubwa”, amesema Bashungwa. Aidha, Bashungwa amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Kagera kumsimamia Mkandarasi anayeendelea na ukarabarati wa barabara ya Lusahunga - Rusumo (km 92) kwa kiwango cha lami ambapo barabara hiyo inauunganisha Mkoa wa Kagera na nchi jirani. Naye, Mbunge wa jimbo la Bukoba Mjini, Stephen Byabato amesema kazi ya ujenzi wa njia nne wa barabara ya Bukoba Mjini unaendelea kwa kasi kubwa na ameiomba Serikali kushughulikia suala la fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa barabara hiyo.

MSOMI ABDUL KATABARO AMETANGULIA ,MARUKU NA BUKOBA WAMLILIA!!

Askofu wa Peoria (USA) alivyowasili Jimboni Bukoba

TAZAMA SEHEMU YA MAPOKEZI MASALIA YA MT.YOSEFU ALLAMANO KWENYE VIWANJA VYA KANISA LA BMC MSHINDO

Inside Tanzania’s $5 Billion Plan to Build a New Capital City

HALI YA UJENZI WA BARABARA YA AMANI FLYOVER - MUEMBELADU WANANCHI WAMPA MAUWA YAKE DK MWINYI

Heche Amshukia Patrobasi Katambi Kufungia Mikutano: 'Hauna Mamlaka Hayo'

ከንቲባ አዳነች አቤቤ በአዲስ ከተማ ክፍለ ከተማ ቅጠል ተራ ተብሎ በሚጠራው አካባቢ ግንባታቸው የተጀመሩ የጋራ መኖሪያ ቤቶችን የግንባታ አፈጻጸም ሂደት ገመገሙ

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG

WHO IS:BUKOBA NI RIO DE JANEIRO,MUNGU ALIWEKA OVERTIME KUIUMBA BUKOBA PROFESA TIBAIJUKA

Why Hydrofoil Boats Disappeared

KADA wa CCM ALIYEUAWA kwa KUCHOMWA KISU BUKOBA - MAMA YAKE ASIMULIA -MBUNGE MUTASINGWA AMSHIKA MKONO

BALAA LA GODBLESS LEMA BUKOBA, AIKAANGA CCM BILA HURUMA, AWAPA ZA USO G55, "NO REFORMS, NO ELECTION"

ትንሳኤ አዲስ

Inside Kenya’s A8 Highway | Rironi to Mau Summit Road Upgrade | New Highway, New Kenya

WANAOTAJWA KUGOMBEA UBUNGE BUKOBA VIJIJINI 2025 HAWA HAPA!

“You’ll Never Be Like Us.” Until 500KG Happened 🔥

John Bolton, former Trump adviser, pleads guilty to retaining classified information

Make Headlights Like Crystal Clear with Aluminum Foil-This Crazy Trick Actually Works!

Mwanasheria Mkuu CHADEMA amjibu waziri Katambi zuio la Mikutano vyama vya siasa.

