BoT KUNUNUA TANI 6 YA DHAHABU – GAVANA TUTUBA

Benki Kuu ya Tanzania imeanza zoezi la ununuzi wa dhahabu kwa lengo la kuchangia maendeleo ya sekta ya madini nchini pamoja na kuongeza akiba ya fedha za kigeni. Akizungumza baada ya ziara katika kiwanda cha kusafisha dhahabu cha Geita (Geita Gold Refinery) na kiwanda cha kusafisha dhahabu cha Mwanza (Mwanza Precious Metals Refinery Co. Ltd), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, amesema kuwa tayari BoT imenunua na kusafisha dhahabu yenye uzito wa kilo 418.