DC MKUDE AZINDUA MRADI WA SOS WA WATOTO WAISHIO NA KUFANYA KAZI MTAANI
Lengo ni kuondoa watoto Mitaani na kuimarisha uwezo wa familia na kuwaunganisha na familia zao Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Modest Mkude amesema kulingana na takwimu za Mei 2026, Mkoa wa Arusha una Jumla ya watoto wanaoishi na kufanya kazi Mtaani wapatao 631, kati yao 94 wakiwa wanalala mtaani, wengi wao wakipatikana kwenye Kituo Kikuu cha mabasi, Kituo kidogo cha Daladala Jiji la Arusha, Soko la Kilombero, Soko kuu na eneo la Mianzini Jijini Arusha. Mhe. Mkude ametoa takwimu hizo hii leo Jumatatu Juni 08, 2026 wakati wa uzinduzi wa mradi wa Shirika la SOS Children Villages wa watoto waishio na kufanya kazi Mtaani, mradi unaotarajiwa kutekelezwa katika Halmashauri za Jiji la Arusha, Meru na Arusha Dc, akisema ni matarajio yake kuwa mradi huo utaenda kuleta suluhu ya changamoto hiyo yenye kutatiza haki na upatikanaji wa malezi na malazi kwa watoto wa Mkoa wa Arusha. "Ni matarajio yetu kama Mkoa kwamba ifikapo 2029, Mkoa wetu uwe wa mfano na kwamba tunatarajia kuondoa watoto wetu wanaoishi na kufanya kazi mtaani na kuwaunganisha na huduma muhimu ikiwemo malezi, malazi, elimu, afya na ujuzi mbalimbali. Na nimesikia kwamba watoto takribani 750 wanatarajiwa kufikiwa nami nisisitize kwamba maeneo yote matatu yanapaswa kusimamiwa kikamilifu ili kwa pamoja tuhakikishe mtoto wa Kitanzania anakuwa salama." Amesema Mhe. Mkude. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la SOS Tanzania Bw. Thomas Kipingili amesema mradi huo wa watoto waishio na kufanya kazi mtaani umelenga kuondoa watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani na kuwaunganisha na familia zao ama mifumo mingine salama ya malezi, kuimarisha uwezo wa familia katika kutoa malezi bora, matunzo na ulinzi wa mtoto kupitia uwezeshwaji wa kiuchumi, kijamii na huduma za msaada wa kisaikolojia na kijamii pamoja na kuimarisha mifumo ya serikali na jamii katika ulinzi wa mtoto ili kumtambua mtoto mapema anapokuwa katika mazingira hatarishi. Kipingili amesema kupitia malengo hayo, wanatarajia kupungua kwa watoto wanaoishi mtaani, kuimarika kwa ustawi wa familia na kuongezeka kwa uwezo katika kulinda watoto dhidi ya ukatili.

LIVE 🔴: LOAN DISBURSEMENT CEREMONY FOR WOMEN, YOUTH, AND PEOPLE WITH DISABILITIES GROUPS - 3RD QU...

MRADI WA SOYA KUWAINUA WAKULIMA 12,500 TUNDURU KIUCHUMI.

IBADA YA SABATO MAALUMU WENYE MAHITAJI MAALUM/tarehe27.06 2026

MERU DC YATOA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU.

SEMAJI AHMED ALLY BAADA YA MCHEZO WA SINGIDA BLACK STARS NINI KINAFUATA/UJUMBE HUU KWA MASHABIKI

RC MAKALLA AIPONGEZA HALMASHAURI YA LONGIDO NA HALMASHAURI ZA ARUSHA KWA KUPATA HATI SAFI🇹🇿

WAZIRI MAKONDA AWAVAA CHADEMA BUNGENI | WANAZUNGUKA KUKINANGA CHAMA CHA MAPINDUZI | SISI WAKUBWA

🔴 Duh: WAZIRI MKUU TAMKO ZITO ATOA | USALAMA WA NCHI, ACHIMBUA MAZITO

MANISPAA YA KIBAHA YATOA TSH MILIONI 991.5 KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU...

LONGIDO YATOA MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 180 KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

BIBI wa SUMBAWANGA amvaa WAZIRI MKUU MWIGULU kwa madai haya MAZITO "sitaki kiwanja nataka hela"

KIBAHA MUNICIPALITY DISBURSES TSH 991.5 MILLION TO SPECIAL GROUPS, BOOSTING LOCAL ECONOMY

June 14, 2026

22 June 2026

UCHAMBUZI MZITO KUHUSU AGIZO LA MARUFUKU MIKUTANO, JE HII INAMAANA GANI?

تلاوة القرآن للدراسة والتركيز 📚🕛 | راحة وطمأنينة | Peaceful Focus Quran | محمد هشام

How US Air Force B 52 Pilot Performed an Emergency Takeoff at Full Speed

The Most Viral Science Videos Ever

TAZAMA DC ARUSHA ATOA UFAFANUZI JUU YA SAKATA LA MGOMO WA DALADALA ARUSHA

