Mkurugenzi mpya CRDB atambulishwa “CV yake imeshiba”

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini (CRDB), Abdulmajid Nsekela ametambulishwa rasmi kwa wafanyakazi na wateja wa benki hiyo Kanda ya Ziwa Mwanza na Shinyanga. Hafla ya kumtambulisha Mkurugenzi huyo aliyechukua nafasi ya Dkt. Charles Kimei imefanyika jana jioni (Januari 29, 2019), katika ukumbi wa Gold Crest Hotel Jijini Mwanza ambapo Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB, Ally Hussein Laay alibeba jukumu la kufanya utambulisho huo.