| KILIMO BIASHARA | Uzalishaji wa mbegu za viazi kwa kutumia vipandikizi vya mashina

Kaunti ya Nyandarua inajulikana pakubwa kwa ukuzaji wa viazi ambapo huzalisha zaidi ya asilimia thelathini ya zao hilo humu nchini. Hata hivyo wakulima hukabiliwa na changamoto za ubora wa mazao na bei duni. Mkulima mmoja kutoka Marekani ameapa kubadilisha taswira hiyo kwa kutumia teknolojia ya kuzalisha mbegu kupitia vipandikizi vya shina. Mwanahabari wetu Denis Otieno anazamia mbinu hiyo ya kilimo kwenye makala ya wiki hii ya Kilimo Biashara.