Mwanafunzi ajipeleka shuleni Shimo la Tewa bila wazazi

Mwanafunzi wa umri wa miaka kumi na minne alilazimika kusafiri kilomita mia nane kutoka Kisii mpaka Mombasa ili kujiunga na shule ya upili ya Shimo la Tewa. Samuel Okeng’o anasema alikumbana na changamoto tele ikiwemo kukosa karo kwani alikuwa na nauli pekee ya kumfikisha Mombasa. Mwanafunzi huyo sasa yuko shuleni lakini anategemea wahisani kumlipia karo na mahitaji mengine ya shule.