LANGO LA MZURI

Kisa cha Lango la Mzuri (Lango Zuri) kinapatikana katika kitabu cha Matendo ya Mitume 3:1–10. Petro na Yohana walikuwa wakielekea hekaluni wakati wa saa ya kusali. Kando ya lango la hekalu lililoitwa Lango la Mzuri, kulikuwa na mtu aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Kila siku aliletwa hapo ili kuomba sadaka kwa watu waliokuwa wanaingia hekaluni. Alipowaona Petro na Yohana, aliwaomba sadaka. Petro akamwangalia na kusema: “Fedha na dhahabu sina, lakini nilicho nacho nakupa; kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.” Petro akamshika mkono wa kuume na kumwinua. Mara miguu na vifundo vyake vikapata nguvu. Akasimama, akaanza kutembea, akaruka-ruka na kumsifu Mungu. Watu wote walimwona na kushangaa sana kwa sababu walimtambua kuwa ndiye aliyekuwa akiomba sadaka kwenye Lango la Mzuri. Mtunzi: Lameck Chacha Instrumental: Lameck Chacha @2026