VIKUNDI 21 VYAPATA MKOPO WA SHILINGI MILIONI 59,PIKIPIKI NA FEDHA YA TASLIMU

Halmashauri ya Wilaya Mtama iliyo katika wilaya na Mkoa wa Lindi imetoa mikopo yenye thamani ya Sh 59,600,000 kwa vikundi 21 vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, George Mbilinyi amesema vikundi 8 vya vijana vilikopeshwa pikipiki, vikundi 10 vya wanawake vilikopeshwa fedha na vikundi vitatu vya walemavu vilipewa fedha. Mbilinyi alisema kwamba mikopo imetolewa kwa mujibu wa sheria inayogusa mikopo ya halmashauri inayotokana na makusanyo ya ndani ambapo Halmashauri zinapaswa kutenga asilimia 10% ya mapato yake ya ndani yanayotokana na vyanzo vyake kwa ajili ya kukopesha vikundi vya Wajasiriamali vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu. Vikundi vya vijana vilivyokabidhiwa mikopo ya pikipiki vinatoka Namupa, Majengo na Mtama. Pikipiki zote hizo zinathamani ya Sh 27,500,000 Akikabidhi pikipiki hizo na fedha kwa vikundi hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Zainab Telack, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga aliwataka wajasirimali walikopa kuhakikisha kwamba wanafanyia kazi zilizokusudiwa ili kujiinua kimapato na kurejesha fedha hizo ili zitumike kuwakopesha wengine. KARIBU COM TV , Television ya Mtandaoni ambayo imejidhatiti katika kuakikisha unapata habari ,Matukio ,Burudani za ndani na nje ya Tanzania kwa uharaka na uwakika. Unaweza kutupata kwenye mitandao ya kijamii kama hivi INSTAGRAM : https://www.instagram.com/p/CPIn1ZNhB... #COM TV #Comtv #Com Tv #LINDI #Tanzania #Liwale #habari #michezo #COM TV #Comtv #Com Tv #COM TV, #Comtv, #Com Tv