MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR ARIDHISHWA NA UJENZI WA BANDARI YA MARUHUBI
Makamun wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya barabara inayoendelea kujengwa nchini zitasaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Ameyasema hayo alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya barabara mbali mbali zinazoendelea kujengwa katika mkoa wa Mijini Magharibi. Amesema uwepo wa miundombinu bora ya barabara inafungua fursa mbali mbali za kiuchumi ikiwemo kutanuka kwa biashara, kuongezeka kwa Pato la Taifa pamoja na kuongezeka thamani kwa maeneo mbali mbalia yaliyopitiwa na barabara hizo. Mhe . Hemed amewahakikishia wananchi wote waliopisha ujenzi wa miradi ya maendeleo kuwa watalipwa fidia zao kulingana na Tathini na viwango vya mali zao zilizoathiriwa na ujenzi wa miradi hio. Aidha, Makamu wa Pili wa Rais ameielekeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuhakisha kuwa wananchi wote waliopitiwa na ujenzi hasa wale waliolipwa fidia zao wanaondoka katika maeneo hayo pamoja na kuandaa utaratibu mzuri wa kuhakikisha wanachi hawarudi tena katika maeneo hayo mara ujenzi wa barabara na miradi mengine utakapokamilika ili kuweka haiba na muenekano mzuri wa miundombinu hio. Sambamba na hayo amewataka wananchi kuendelea kuwa wavumilivu na kutoa ushirikiano kwa wakandarasi wa ujenzi wa miundombinu hio ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na kukamilisha ndani ya muda uliopangwa. Hata hivyo, amewataka wakandarasi wanaojenga barabaraha hizo kuongeza kasi ya ujenzi ili ziweze kukamilika kwa wakati na kwa viwango vya hali ya juu ili wananchi waondokane na nchangamoto ya usafiri na usafirishaji. Nae Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Dkt. Khalid Salum Muhammed amesema ujenzi unaoendelea wa barabara za Mjini unatarajiwa kukamilika kabla ya mashindano ya Afkon kuanza ili kutoa fursa kwa wageni watakaoingia nchini kufurahia huduma mbali mbali wakati wote watakapokuwepo Zanzibar. Dkt. Khalid amesema Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ipo katika matayarisho ya ujenzi wa barabara ya Tunguu hadi Makunduchi ambayo itarahisisha zaidi huduma ya usafiri na usafirishaji na kufungua fursa za kiuchumi katika maeneo hayo. Akizungumzia suala la ulipaji wa fidia, waziri Khalid amesema kwa asilimia kubwa wananchi waliopitiwa na miundombinu ya barabara tayari wamekwisha kulipwa fidia zao na waliobakia Wizara inakamilisha taratibu za tathmini ili waweze kulipwa na shughuli za ujenzi ziweze kuendelea. Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na uchukuzi Mhandisi ALI SAID BAKARI amesema barabara zinazojengwa katika Mji wa Zanzibar zinatarajiwa kukamilika mwezi Disemba 2026 ambazo zitajukuisha Taa za barabaranj, mitaro ya kupitishia maji na njia za watembea kwa miguu jambo ambalo litatatua changamoto ya msongamano wa magari na vyombo vyengine vya usafiri katika maeneo ya Mji wa Zanzibar. Mhandisi ALI amesema kwa upande wa barabara ya juu (Flyover) ya Amani inatarajiwa kukamilika mwezi wa Kumi (10) na kuanza kutumika rasmi na kusema kuwa wizara inaendelea kuwasimamia vyema wakandarasi wanaojenga barabaraha hizo ili kuhakikisha zinakamilika ndani ya muda uliopangwa. Wakati huo huo makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alikagua maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Maruhubi ( MPIGADURI ) na kusema kuwa ameridhishwa na kazi kubwa inayofanywa na Shirika la Bandari Zanzibar wakishirikiana na Kampuni ya ZF DEVCO ya kuhakikisha bandari hio inakamilika na kuanza kutoa huduma jambo litakalopunguza changamoto ya ufinyu wa Bandari na kupunguza msongamano wa meli zinazosubiri kushusha mizigo. Mhe. Hemed ameiagiza Wizaraya ya Maji, Nishati na Maadini kuruhusu upatikanaji wa vibali vya mchanga pamoja na Wizara ya Uchumi wa Buluuu kuhakikisha wanawawekea mazingira mazuri wavuvi waliopo katika maeneo hayo ili waweze kupisha ujenzi wa PHASE ONE B uweze kuendelea. Amewataka ZPC kuhakikisha kituo cha kukagulia na kupimia mizigo kunafanya kazi kwa ufanisi kwa kuhakikisha abiria na mizigo yote inayoingia na kutoka bandarini hapo inafanyiwa ukaguzi ili kulinda mapato ya nchi lakini pia kuepusha uingiaji wa bidhaa zisizokuwa salama kwa matumizi ya binaadamu. Katika ziara hio Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amekagua ujenzi wa barabara ya Viwanja vya Magereza - kwa Mchina,(Othman Maalim) Mwanakwerekwe Makaburini- Magomeni hadi Kariakoo, Flyover amani, barabara ya Amani Mikunguni hadi Biziredi, barabara ya Mnazi mmoja Malindi hadi Kinazini na barabara ya ZRA- Fumba pamoja na kukagua Bandari ya Maruhubi ( MPIGADURI ) Imetolewa na Kitengo cha Habari ( OMPR ) Leo tarehe…04 / 07 / 2026

RAIS SAMIA, AKIWEKA JIWE LA MSINGI LA MRADI WA UJENZI WA RELI YA KISASA (SGR) TABORA KIGOMA

Iran na Marekani njia Panda .Katika Dira ya Dunia TV

Rais Samia Kwenye Uzinduzi wa Ujenzi SGR Kigoma, 'Tunaifufua Kigoma na Kuirudishia Hadhi Yake'

TUFUNUWE KITABU (SILSILA 25): Zanzibar: The Last Years of the Protectorate cha Maulid Mshangama

Imiterere y’inzu 2000 ziri kubakwa i Nyabisindu | Sobanukirwa uyu mushinga uzahindura Kigali

NI NDE WATEKEREZAGA KO IRAN YAMARA IKI GIHE CYOSE MU NTAMBARA? // KNC NA MUTABARUKA

WAZIRI LEILA ATOA AGIZO ZITO KWA WALIMU BAADA YA MSAADA WA ALGERIA KUTUA ZANZIBAR

RAIS SAMIA AFANYA UZINDUZI WA MELI KIGOMA/

KWA HESABU HIZI TRUMP AMEPIGWA HASARA NZITO SANA NA IRAN | UKWELI UMEFICHWA VIFO VYA WANAJESHI WAKE

Minisita Byamukama Akawangamudde, Ensimbi Ezirina Okukola Busega - Mpigi Express Zabbibwa #Gambuuze

KESI YA LISSU KUENDELEA LEO/RAIS SAMIA ASISITIZA AMANI UZINDUZI WA MIRADI KIGOMA/AFISA ARDHI AUAWA

ALI KARUME AIBUA MAPYA, ASEMA CCM HAIJAWAHI KUSHINDA UCHAGUZI ZANZIBAR, WANAKAA MADARAKANI KWA UBABE

How Luxury Apartments Are Changing Nairobi Forever

This City in Tanzania will host AFCON 2027 Games. A drive on 16km Arusha Dual highways

OMO makes clear its position on land and rights of Zanzibari | ZANZIBAR DECIDES 2025

Maridhiano Mapya Zanzibar: Je, Makubaliano ya CCM na ACT Wazalendo Yatadumu?

Inside A 12 BILLION KSH Kenya Airways Boeing 777-300 ER !!

Ansbert Ngurumo ataadharisha - Maamuzi ya Jumuiya ya Madola kuhusu Kesi ya Lissu

The Final Hours of GEDAM SEFER! Piassa’s Oldest Heart is Turned to Dust, Addis Ababa 2026

