WAZIRI WA ULINZI DKT. STERGOMENA TAX Awaaga Watumishi wa Wizara na Kuwapa Ujumba huu...

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax tarehe 16 Oktoba, 2025 amefanya mazungumzo na Wafanyakazi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambapo pamoja na mambo mengine ametumia wasaa huo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa Utumishi Kikatiba katika wizara ya Ulinzi kufuatia Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 nchini kote. Waziri Stergomena amezungumza na kuwaaga Wafanyakazi hao katika Ukumbi wa Mabele wa Jijini Dodoma na kuwashukuru wafanyakazi wa Wizara kwa ushirikiano wao waliomuonyesha na kumpatia katika kipindi chote alichohudumu kama Waziri wa Ulinzi. Amewashukuru wafanyakazi hao kwa mshikamano waliouonyesha, kujituma, uadilifu na moyo wa kizalendo na Weledi wa kila mmoja kwa nafasi yake waliomuonyesha kwa muda wote wa utumishi wake. “Waswahili husema Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu kauli hii imejidhililisha wazi katika Utendaji wetu”, akaongeza, “hata ukiwa na uwezo mkubwa kiasi gani ni vigumu kufanikisha mambo peke yako hususani mambo makubwa, hata ukijigamba kuwa umefanikisha peke yako uhalisia utaonyesha kuwa ipo michango kwa waliokusaidia au ulioshirikiana nao hivyo basi natambua mchango wa kila mmoja wenu” alisisitiza Waziri Stergomena Tax. Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt Stergomena, akachukua fursa hiyo pia kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuhudumu katika nafasi hiyo adhimu kama Wazari wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mara mbili Septemba 2021 hadi Oktoba 2022 na mara ya pili Agosti 2023 hadi sasa Oktoba 2025 ambapo amehudumu katika Wizara ya Ulinzi na JKT kwa jumla miaka mitatu. Awali akimkaribisha Waziri wa Ulinzi ili aongee na wafanyakazi, Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na JKT Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe alimpongeza Waziri Stergomena kwa uongozi wake mahiri na kusema anajivunia kwa kuwa amekuwa Katibu Mkuu wa kwanza kuongozwa na Waziri wa Ulinzi na JKT wa kwanza Mwanamke tangu nchi yetu ipate Uhuru. Hafla ya Waziri wa Ulinzi na JKT kuongea na kuwaaga Wafanyakazi ilihudhuriwa pia na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Ulinzi, Makamishna wa Wizara, Maafisa Jenerali, Maafisa wakuu na wadogo na askari pamoja na watumishi wa umma wa Wizara ya Ulinzi na JKT. #wizarayaulinzi #jwtz #jkt #DktStergomenaTax #WaziriwaUlinzi

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | 30.06.2026 | Jioni | Swahili Habari leo | Podcast
▶︎

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | 30.06.2026 | Jioni | Swahili Habari leo | Podcast

"WAZIRI AMEONGEA KITU AMBACHO HAKIJUI" MADELEKA AMPASUA KATAMBI BILA UOGA
▶︎

"WAZIRI AMEONGEA KITU AMBACHO HAKIJUI" MADELEKA AMPASUA KATAMBI BILA UOGA

WAZIRI WA ULINZI NA JKT , Dkt Stergomena Tax, Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni Tarh 20 Mei 2025
▶︎

WAZIRI WA ULINZI NA JKT , Dkt Stergomena Tax, Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni Tarh 20 Mei 2025

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | 30.06.2026 | Mchana | Swahili Habari leo | Podcast
▶︎

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | 30.06.2026 | Mchana | Swahili Habari leo | Podcast

LIVE: Macron greets Thailand’s king and queen during state visit to France
▶︎

LIVE: Macron greets Thailand’s king and queen during state visit to France

LHRC Yamtolea Uvivu Waziri Katambi: "Katazo la Mikutano ya Siasa ni Kinyume Cha Katiba"
▶︎

LHRC Yamtolea Uvivu Waziri Katambi: "Katazo la Mikutano ya Siasa ni Kinyume Cha Katiba"

Hotuba ya uzinduzi wa Bunge la 11 dodoma Nov 20,2015
▶︎

Hotuba ya uzinduzi wa Bunge la 11 dodoma Nov 20,2015

DKT.SLAA AWA MBOGO WAZIRI MKUU ANATULETEA POROJO,AJIBU VIKALI KAULI YA MWIGULU KUELEKEA MAANDAMANO77
▶︎

DKT.SLAA AWA MBOGO WAZIRI MKUU ANATULETEA POROJO,AJIBU VIKALI KAULI YA MWIGULU KUELEKEA MAANDAMANO77

🔴#LIVE:ZUIO MIKUTANO ya VYAMA vya SIASA LAIBUA MJADALA/VYAMA VYAHOJI/NINI KINAFUATA?/KUHOJIWA/KAMATI
▶︎

🔴#LIVE:ZUIO MIKUTANO ya VYAMA vya SIASA LAIBUA MJADALA/VYAMA VYAHOJI/NINI KINAFUATA?/KUHOJIWA/KAMATI

WAZIRI MAKONDA AWAVAA CHADEMA BUNGENI | WANAZUNGUKA KUKINANGA CHAMA CHA MAPINDUZI | SISI WAKUBWA
▶︎

WAZIRI MAKONDA AWAVAA CHADEMA BUNGENI | WANAZUNGUKA KUKINANGA CHAMA CHA MAPINDUZI | SISI WAKUBWA

🔴#LIVE: RAIS SAMIA ANAFUNGUKA KILA KITU MUDA HUU KUELEKEA SABA SABA, GAWIO NA MICHANGO..............
▶︎

🔴#LIVE: RAIS SAMIA ANAFUNGUKA KILA KITU MUDA HUU KUELEKEA SABA SABA, GAWIO NA MICHANGO..............

MATOKEO YA USAILI WA MAHOJIANO (ORAL) NA WALIOPO KWENYE KANZIDATA KUANZA KUWEKWA WAZI HIVI KARIBUNI
▶︎

MATOKEO YA USAILI WA MAHOJIANO (ORAL) NA WALIOPO KWENYE KANZIDATA KUANZA KUWEKWA WAZI HIVI KARIBUNI

🅻🅸🆅🅴.....🔴#LIVE; WAKILI PETER MADELEKA ANAZUNGUMZA MAZITO MUDA HUU..
▶︎

🅻🅸🆅🅴.....🔴#LIVE; WAKILI PETER MADELEKA ANAZUNGUMZA MAZITO MUDA HUU..

Meet the Former CIA Agent Who Wants to Abolish the CIA
▶︎

Meet the Former CIA Agent Who Wants to Abolish the CIA

🔴 #ZBCLIVE :- BARAZA LA 11 LA WAWAKILISHI - ZANZIBAR - MKUTANO 03 KIKAO CHA 36 NO 3
▶︎

🔴 #ZBCLIVE :- BARAZA LA 11 LA WAWAKILISHI - ZANZIBAR - MKUTANO 03 KIKAO CHA 36 NO 3

Rymanowski, Miller: UPA-dek przyjaźni?
▶︎

Rymanowski, Miller: UPA-dek przyjaźni?

"Keep Supporting the Venezuelan People": Thousands Missing as Earthquake Rescue Efforts Continue
▶︎

"Keep Supporting the Venezuelan People": Thousands Missing as Earthquake Rescue Efforts Continue

WAZIRI WA ULINZI NA JKT AMKABIDHI MKUU WA MAJESHI WA KWANZA MSTAAFU TANZANIA GARI JIPYA LA KISASA
▶︎

WAZIRI WA ULINZI NA JKT AMKABIDHI MKUU WA MAJESHI WA KWANZA MSTAAFU TANZANIA GARI JIPYA LA KISASA

HECHE: MKE WA TUNDU LISSU NA DADA YAKE POLE POLE WAMEUWASHA MOTO BUNGE LA ULAYA
▶︎

HECHE: MKE WA TUNDU LISSU NA DADA YAKE POLE POLE WAMEUWASHA MOTO BUNGE LA ULAYA

LIVE KASRI : KUJIUZURU KWA WAZIRI MKUU WA UINGEREZA, SAKATA LA TOZO BUNGENI,ZIARA YA RAIS WA NAMIBIA
▶︎

LIVE KASRI : KUJIUZURU KWA WAZIRI MKUU WA UINGEREZA, SAKATA LA TOZO BUNGENI,ZIARA YA RAIS WA NAMIBIA