Ibada Maalum ya shukrani ya Kustaafu kwa mchungaji Philemon Tibanenason

Kanisa la Pentekoste Tanzania lilianza mwaka 1949. Wakati huo kanisa hili lilikuwa likiitwa Swidish Free Mission. Mwaka 1971 Kanisa lilibadilishwa jina na kuitwa Kanisa la Pentekoste Dar es Salaam kabla ya Kubadilishwa tena na kuomba kubadilishwa na kuitwa Kanisa la Pentekoste Tanzania mwaka 1996 Kanisa la Pentekoste Tanzania Lilianza kuwa na utaratibu wa uongozi wa kuwa na mwangalizi mkuu kama kiongozi mkuu wa kanisa, ambapo Mchungaji Philemon Tibanenason akiwa mwanzilishi na Mwangalizi mkuu. Mchungaji Philemon Tibanenason alijiunga na Kanisa la Pentekoste Tanzania tarehe 10/12/1969 na mnamo tarehe 12/03/1972 alisimikwa kuwa mchungaji wa kanisa katika Parish ya jiji, Lindi street. Mchungaji Philemon Tibanenason aliteuliwa kuwa mwangalizi wa kanisa mpaka mwaka 2023 alipostaafu rasmi na kukabidhi uongozi kwa viongozi wapya. Leo, tumekusanyika hapa katika Kanisa la Pentekoste Kiluvya, likiwa ni moja ya Parishi za makanisa yetu, na tumekuja kumshukuru Mungu kwa utumishi wa mtumishi wake mchugaji Philemon Tibanenason katika Kanisa la Petekoste Tazania. Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa safari ya utumishi wake katika kipindi chote cha miaka 58 ya utumishi wake. Mchungaji Philemon Tibanenason amefanya kazi kubwa sana ambapo zaidi ya makanisa 100 ya KLPT yameenea nchi nzima.