CRDB YAIMARISHA AFYA ZA WAFANYAKAZI KUPANDISHA TIJA YA KAZI
CRDB YAIMARISHA AFYA ZA WAFANYAKAZI KUPANDISHA TIJA YA KAZI Benki ya CRDB imeendelea kuwekeza katika ustawi wa wafanyakazi wake kwa kuendesha programu ya afya na mazoezi (Wellness Programme) inayowakutanisha zaidi ya wafanyakazi 800 wa kanda za Dar es Salaam na Pwani kwa ajili ya vipimo vya afya, elimu ya lishe na mazoezi, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza tija na kupunguza athari za magonjwa yasiyoambukiza mahali pa kazi. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Brusi Mwile, amesema benki inaamini kuwa wafanyakazi wenye afya bora ndiyo msingi wa utoaji wa huduma zenye ubora na ukuaji endelevu wa taasisi. Naye Meneja wa Rasilimali Watu wa CRDB, Timothy Fasha, amesema programu hiyo ambayo imefikia msimu wake wa sita na kufanyika kwa mwaka wa nane sasa, inalenga kuwajengea wafanyakazi utamaduni wa kufanya mazoezi na kufahamu vihatarishi vya magonjwa yasiyoambukiza kama shinikizo la damu, kisukari na saratani,amesema mpango huo unatekelezwa katika matawi yote ya benki nchini, Zanzibar na Burundi, huku wataalamu wa afya na lishe wakitoa huduma na ushauri wa kitaalamu. Kwa upande wake, Msimamizi wa Idara ya Wellness kutoka kampuni ya Care Health & Hospitality Services, Jovicus Masalu, amesema ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza miongoni mwa wafanyakazi wa ofisini limekuwa changamoto inayopunguza uzalishaji, hivyo ushirikiano wao na CRDB unalenga kutoa vipimo vya afya, ushauri wa lishe na kuhamasisha mabadiliko ya mtindo wa maisha ili kuimarisha afya za wafanyakazi na familia zao. Programu hiyo imejumuisha vipimo vya shinikizo la damu, sukari, uzito, urefu na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa madaktari bingwa, wataalamu wa lishe na wakufunzi wa mazoezi, huku CRDB ikisisitiza kuwa uwekezaji katika afya ya wafanyakazi ni sehemu ya mkakati wa kujenga nguvu kazi yenye ufanisi, kupunguza gharama za matibabu na kuongeza tija ya huduma za benki kwa muda mrefu.

CRDB,CCBRT WAUNGANA KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI KWA WATU WENYE ULEMAVU

ROUTES, PORTS, MÉTRO, GRAND INGA : LES GRANDS TRAVAUX DE LA RDC

CRDB YAPELEKA TABASAMU KWA MAPACHA WATANO NA WAZAZI WAO

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG

KAMATI YAWASILISHA MAPENDEKEZO KUWAINUA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI

From Mega Ambition to Real Infrastructure Delivery | Brook Taye, CEO of Ethiopian Investment Holding

Incubators Machines Bora zaidi Matokeo ya Uanguaji ni 90% Full Automatic +255 713 852 296

CRDB YAKABIDHI JEZI, MEDALI NA MAKOMBE BUNGE BONANZA

NaCoNGO, KUWAKUTANISHA WADAU WA MASHIRIKA DODOMA OCTOBER 20 22 2026

Démission, Revirement de Diomaye...: Grosses Révélations de Cheikh Thioro Mbacké

Deported To Nigeria With British Kids- SHOCKING STORY!

I Went Back to Afghanistan in 2026... The Change Shocked Me 🇦🇫

LOST EARNINGS - UZOR ARUKWE, PAMELA OKOYE, Nigerian Movies 2026 Latest Full Movies

Sh. Isa Ma: Answering revert questions

تلاوة القرآن للدراسة والتركيز 📚🕛 | راحة وطمأنينة | Peaceful Focus Quran | محمد هشام

URUS WAJA NA NJIA YA KUONGEZA NG'OMBE KWA MFUGAJI

KITUO KIPYA CHA HUDUMA KWA WAFANYAKAZI WAHAMIAJI CHAZINDULIWA DAR

UCHAMBUZI MZITO KUHUSU AGIZO LA MARUFUKU MIKUTANO, JE HII INAMAANA GANI?

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI YA ASKARI WA ZIMAMOTO KOZI NAMBA 6/2026

