WAKULIMA WA MWANI WALIA NA BEI YENYE TIJA

Wakati Tanzania ikichagiza ajenda ya Uchumi wa buluu kwa kuzingatia mnyororo wa thamani kwenye sekta ya uvuvi na rasilimali Bahari, wakulima na wachuuzi wa kilimo cha mwani katika Kijiji cha Moa, Wilayani Mkinga mkoa Tanga wameiomba serikali na wadau kuzingatia bei yenye tija kwenye mazao ya mwani ili kuweza kujiimarisha kiuchumi. Taarifa ya HABABI MOHAMMED kutoka Wilayani Mkinga mkoani Tanga inafafanua zaidi.