WANGONI WACHACHAMAA WATAKA KICHWA CHA NDUNA SONGEA MBANO

Mjadala mzito umezuka katika siku tatu za tamasha la kumbukizi la Mashujaa wa Vita vya Majimaji ambalo hufanyika kila mwaka Makumbusho ya Taifa ya Majimaji ya Songea kuanzia Februari 25,26 na kilele chake ni Februari 27.Wasomi wa vyuo vikuu wamekuwa na maoni tofauti kuhusu kichwa cha Kiongozi wa wangoni Songea Mbano ambacho kilikatwa na kuchukuliwa na wajerumani mwaka 1906.