May 19, 2026

Kikosi cha KMKM Zanzibar leo tarehe 18/05/2026 kimefanikiwa kuopoa mwili wa Marehemu Adinani Abdalla Bilal Mkaazi wa kibweni mwenye umri wa miaka 20 Ambaye Amezama katika Bahari ya kibweni yuma ya hotel ya Golden tulip. Mwili wa Marehemu huyo ulikabidhiwa katika Hospitali ya Chumbuni kwa Ajili ya uchunguzi zaidi . Aidha Mkuu wa Mawasiliano katika kitengo cha Uzamiaji na Uwokozi KMKM L/t. Malik Makame Hussen Amewataka vijana kwa kuchukuwa Tahadhar zaidi Mapema juu ya Suala la kuogelea na pindi watakapopata Maafa yoyote kutoa taarifa katika kikosi cha KMKM kwa hatua zaidi.