VUTA NI KUVUTE SAKATA LA MAJI MBEZI MSUMI, WANANCHI WAGOMEA MRADI WA BILION 18 WAZIRI ATOA AGIZO
Kampuni ya Mwananchi Communications LTD wasambazaji wa magazeti ya Mwananchi, Thecitizen na Mwanaspoti Tanzania. Wakati Serikali ikitangaza kujenga mradi wa maji wa Sh18 bilioni, wakazi wa Mtaa wa Msumi, Kata ya Mbezi, jijini Dar es Salaam wamegoma kuchimbiwa visima vya muda mfupi wakati wakisubiri mradi huo unaohusisha kutandaza mabomba na kujenga tenki la lita milioni sita. Msingi wa kugomea kuchimbiwa visima na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (Dawasa) ni kuchoshwa na ahadi za muda mrefu zinazotolewa. Hayo yametokea leo Alhamisi, Juni 20, 2024 baada ya Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew kufika katika mtaani humo na kupokewa na mabango ya kulalamikia ukosefu wa majisafi. Hatua hiyo ya Kundo kufika eneo hilo kujionea hali halisi, inakuja ikiwa ni siku tatu zimepita tangu Gazeti la Mwananchi lilipotoa habari maalumu ya adha ya maji kwa baadhi ya maeneo jijini Dar es Salaam ikiwaemo Mtaa wa Msumi ambao baadhi wanalazimika kutumia saruji ili kuyasafisha. "Nimeyaona mabango, mmesema mmechoka kudanganywa masuala ya maji," amesema Kundo wakati akisoma moja ya bango. Kundo amesema ametumwa na Rais Samia Suluhu Hassan, kwamba Serikali imelenga kumtua ndoo mwanamke kichwani ili wasitembee umbali mrefu kutafuta maji. "Wakati tunakuja tumesimamishwa Mshikamano wananchi wakasema wanataka maji, tukasimamishwa tena wakasema wanataka maji, nimekuja hapa nimepokewa na mabango, yakisema tumechoka kudanganywa," amesema

Wananchi wanaoishi Eneo la "Razaba-Makurunge Bagamoyo" Wamlilia Rais Samia Wasiondolewe Kwenye M..

WAKILI MADELEKA acharuka AJIPANGA KUKIBURUZA CHUO CHA ARDHI MAHAKAMANI "WEWE UTAKIFUNGA CHUO"

KIJANA WA MIAKA 32 ANAYEMILIKI MALORI 7 YA FAW, ALIKOPA KWA KUTUMIA NYUMBA AKAMFICHA MKEWE

EXCLUSIVE INTERVIEW PART 1 || MAGORI AFUNGUKA MAZITO MSIMBAZI

DENIS MPAGAZE: Mfahamu EMILIO MWAI KIBAKI / Bingwa Wa Siasa Aliyeingia IKULU Kwa Vyama Tofauti

NEEMA YA MAJI NGERENGERE MOROGORO ZAIDI YA WANANCHI 9500 WAPATA MAJI SAFI NA BARIDI

NARWANYE KWA IDI AMIN MBERE YO KUJYA MU NKOTANYI||UBUNDI IRIYA MBUNDA NINI NIYO YANJYE||AFANDE KING

#live BUNGE LA KUMI NA TATU, MKUTANO WA TATU, KIKAO CHA AROBAINI NA TANO

LIVE : RAIS DKT. JOHN P. MAGUFULI AKIWA NJIANI KURUDI DAR ES SALAAM

🔴#LIVE: TEC WANATOA TAMKO YALIYOTOKEA OKTOBA 29 ,NA MSIMAMO MKALI...

WANANCHI WA CHANIKA WALALAMIKA KUUZIWA MAENEO YAO

🔴LIVE: MWENYEKITI TAIFA ACT WAZALENDO OTHMAN MASOUD ANAFUNGUKA MUDA HUU

Bunge la ulaya lapiga kura ya mwisho kuzuia misaada na ufadhili kwa Tanzania Wakili garubindi aibuka

MCHUNGAJI MSIGWA: WATAWALA WAKUBALI MAKOSA KUELEKEA MARIDHIANO YA KWELI

#Live: MJADALA WA PPP KUHUSU MAGEUZI SEKTA YA AFYA NCHINI KUELEKEA DIRA 20250

LIVE: OTHUMAN MASOUND ANATOA TAMKO, nini kinaendelea ACT WAZALENDO.....

DON'T DARE KENYANS,WE DONT WANT THAT FACILITY LET USA TAKE IT TO THEIR COUNTRY.Ndindi Nyoro on Ebola

LIVE : RIPOTI NZITO YA LHRC YAFICHUA UKWELI WA OKTOBA 29 – na yote ya 2025

PARESSO AJITOLEA KUJENGA OFISI ZA CCM KARATU

