Shamirisho|Yambwa

Shamirisho /Yambwa Shamirisho ni jina la kitu au mtu ambalo huathiriwa na kitenzi katika sentensi na huja baada ya kitenzi kikuu. Aina za Shamirisho 1.Shamirisho kipozi /yambwa tendwa. Huonyesha kile kinachotendwa katika sentensi; Huonyesha kile ambacho hupokea athari ya kitenzi moja kwa moja. Mfano:Mwalimu anaandika sentensi, Wazazi wanawafunza watoto. Katika sentensi hizi mbili, sentensi na watoto ni kipozi. 2.Shamirisho kitondo /Yambwa tendewa. Huonyesha kile ambacho hupokezewa athari ya kitenzi katika sentensi. Mfano :Mama anampikia mtoto chakula, Kibarua alimlimia mkulima shamba. Katika sentensi hizi mbili, mtoto na mkulima ni kitondo au yambwa tendewa. 3.Shamirisho ala /kitumizi. Huonyesha kile ambacho husaidia kutendeka kwa jambo au kitendo fulani katika sentensi. Mfano :Mama anampikia mtoto chakula kwa sufuria, Kibarua alimlimia mkulima shamba kwa jembe.