1. MADHARA YA KUBAKI UKIKAA KATIKA MAZINGIRA/WATU AMBAO MUNGU AMEKWAMBIA USIKAE

Mwl. Walter M. Mrisha Septemba 2025 1.MALENGO YA SOMO 1.1.Kujua njia au mazingira ambayo shetani ameyatengeneza ili ushindwe kufanya au kufikia malengo ya Mungu katika safari yako hapa duniani ya kwenda mbinguni. 1.2.Kufahamu mipango ya Mungu anayoitumia ili kuilinda nafsi yako kusudi iweze kupokea baraka alizokusudia uzipokee katika Ufalme wake hapa duniani na mbinguni. 2.UTANGULIZI 2.1.Msingi wa somo: Hes. 33:50-56; Yos. 23:12-13 2.2.Maana ya neno mazingira ya kiroho Kwa kadiri neno hili litakavyotumika katika somo, mazingira ya kiroho ni hali ya kiroho iliyoko katika eneo fulani inayosababishwa na aina ya maisha ya kiroho wanayoishi watu wa eneo hilo. Mfano wa mazingira ya kiroho: mahusiano, tabia, tamaduni, kampuni, taasisi, biashara, dini, mtandao, ardhi, ulimwengu huu n.k 2.3.Ili Mungu akufanikishe katika eneo alilokusudia kukuweka, lazima uhakikishe unashirikiana naye katika kutengeneza mazingira mazuri ya kiroho ukiwa kakatika eneo hilo; kusudi mazingira yasikukwamishe kupokea baraka zake. 3.MADHARA YA KUBAKI UKIKAA KATIKA MAZINGIRA YA KIROHO AMBAYO MUNGU AMEKWAMBIA USIKAE 3.1.Kumzuia Mungu asitekeleze kwa ufanisi mipango na malengo yake mema aliyonayo juu ya maisha yako. 3.2.Kushindwa kustahimili nguvu za upinzani wa shetani zilizoko katika mazingira hayo kutokana na upungufu wa nguvu za kiroho ndani yako (1Kor. 10:13; Mdo. 1:4, 8) ******************************* Pata Notes zote za somo: https://wanafunziwayesuonline.blogspo... MAWASILIANO ------------------------ MAOMBI - MAOMBEZI - USHAURI - MAFUNDISHO - USHUHUDA - SADAKA +255 714 766 148 / +255 620 576 148 Website: www.wanafunziwayesuonline.blogspot.com Facebook: Wanafunzi wa Yesu E-mail: [email protected] #InjiliYaUtakatifu #HudumaYaNeno #YesuNiBwana #NenoLaMungu #OkokaSasa #YesuMwokozi #FungaNaKuomba #NguvuYaMaombi #MaishaYaUtakaso #KristoNdaniYetu #TakatifuKamaYesu #WatakatifuWaBwana #UongoziWaRohoMtakatifu #Usichelewe #WanafunziWaYesu #UfunuoWaNeno #InjiliYaKweli #BibliaInasema #TumtangazeYesu #YesuArudiTena