RAIS MWINYI AWAKA ZANZIBAR KILA SIKU MAMBO MAPYA DUNGA KUMENOGA

7 AGOSTI 2024 WILAYA YA KATI - MKOA KUSINI UNGUJA RAIS MWINYI UWEKAJI JIWE LA MSI NGI – DUNGA ZUZE Rais wa Zanzibar na Mweyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar itapiga hatua muhimu katika sekta ya Uwekezaji kwa kuwa na Maeneo ya Uwekezaji yenye Miundombinu yote itakayowavutia Wawekezaji kuja kuwekeza nchini. Rais ametoa tamko hilo leo tar 07 Agosti 2024 wakati wa uwekaji wa jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barbara kaitka eneo la Viwanda Dunga. Dk, Mwinyi amesema hatua hiyo inalenga kuchochea Maendeleo ya kiuhumi, Uwekezaji na kupunguza Umasikini kwa wananchi kwa kuongeza kipato Chao. Amefahamisha kuwa Uwekaji wa jiwe hilo la msingi ni utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2050 na ilani ya CCM na Mpango wa Maendeleo wa ZanzibarZADEP unaolenga kukuza mchango wa sekta ya Viwanda katika Uchumi. Rais Mwinyi amesisitiza kuwa Mkakati wa kuimarisha mtandao wa Barabara ni kuunganisha maeneo yote ya Uzalishaji na masoko, kupunguza gharama za Usafirishaji katika maeneo ya Viwanda. Akitoa taarifa ya kitaalamu ya Ujenzi huo Katibu Mkuu wa wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Nd, Fatma Mbarouk ameyataja maeneo ya Dunga Zuze,Pangatupu na Chamanangwe Pemba kuwa ni maeneo makuu ya kimkakati ya Uwekezaji wa Viwanda yanayoimarishwa ili kuwavutia Wawekezaji.. Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mh, Omar Said Shaaban amesema kinachofanyika sasa ni utekelezaji wa sera ya Viwanda va 2019-2026 na tayari Wizara imeandaa mpango maalum wa kutathmini changamoto zinazoiathiri delta ya Viwanda nchini. Rais Mwinyi alishuhudia Utiaji wa saini wa miradi ya Ujenzi wa Kiwanda cha dawa na chanjo za binaadamu , Ujenzi wa Maabara zitakazohusika na Ukaguzi wa bidhaa za viwandani na Kiwanda cha Uunganishaji wa Magari .