WAZIRI MKUU DKT MWIGULU ALIVYOJIBU HOJA ZA MZINDAKAYA AKIWA ZIARANI RUKWA.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amejibu na kutoa maelekezo mbalimbali kuhusu hoja zilizowasilishwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Jacqueline Mzindakaya, wakati wa ziara yake mkoani humo. Hoja hizo zilihusu sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo miundombinu, afya, biashara na kilimo, ambapo Mheshimiwa Mzindakaya alizipaza sauti kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Rukwa. Kuhusu suala la miundombinu ya usafiri wa anga, awali Mheshimiwa Mzindakaya alihoji bungeni maendeleo ya ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Sumbawanga. Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, alieleza kuwa maandalizi ya mwisho yanaendelea na kwamba majaribio ya kurusha ndege yataanza hivi karibuni. Hatua hiyo ilidhihirika Machi 8, 2026 wakati Waziri Mkuu alipotua katika uwanja huo akiwa ziarani mkoani Rukwa. Katika sekta ya afya, Mheshimiwa Mzindakaya aliiomba Serikali kujenga Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Rukwa ili kupunguza adha ya wananchi kusafiri mikoa mbalimbali kutafuta huduma za madaktari na kutumia gharama kubwa za matibabu. Akijibu hoja hiyo, Waziri Mkuu aliagiza mamlaka husika mkoani Rukwa kuwasilisha rasmi ombi hilo Serikalini ili liweze kufanyiwa kazi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050. Aidha, katika sekta ya biashara, Mbunge huyo aliwasilisha ombi la kufungwa kwa taa katika Soko la Namanyere (Majengo) Wilayani Nkasi, ili kuwawezesha wanawake wajasiriamali wadogo wadogo kufanya biashara zao hadi nyakati za usiku kwa usalama zaidi. Katika sekta ya kilimo, Mheshimiwa Mzindakaya alihoji utekelezaji wa mradi wa skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Katongolo. Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa David Silinde, alieleza kuwa serikali inaendelea kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha unakamilika na kuwanufaisha wananchi. Akihitimisha, Mheshimiwa Jacqueline Mzindakaya alimshukuru Waziri Mkuu kwa namna anavyosikiliza na kujibu hoja za wananchi. #gachitvonlineupdates #gachitv #gachitvonline

live: KIMENUKA WAZIRI MKUU amtumbua MTUMISHI ofisi ya RC "ameshindwa familia yake ataongozaje watu"

NIPASHE ~ JUNE 11TH, 2026

NILIMUOMBA KAKA ANILIPIE KODI YA MIEZI MITATU NIBAKI DAR | NIMETOKA KIJIJINI SANA | MAJID NSEKELA

JOHN MBADI GETS BOOED DURING FINANCE BILL PRESENTATION AS RUTO HIDES IN FINLAND!

US forces shot down Iranian drones near Strait of Hormuz

TUONGEZE KASI NA UKARIBU ZAIDI NA WANANCHI-DKT. GWAJIMA.

Ghana Just Got 1,840 Agricultural Machines From Belarus Deal — Here's What Happens Next

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AWAMKALI,ATOA MSIMAMO BAADA YA WANANCHI KUDHURUMIWA HAKI ZAO

U.S. military fires on tanker in Gulf of Oman

Apparent Trump Protest Phrase ‘86 47’ Etched Into National Mall

GOOSEBUMPS! THE WORLD STOPPED TO WATCH MOROCCO BEAT BRAZIL FOR THE FIRST TIME IN HISTORY

MANARA ALIVYOMBANA WAZIRI KATAMBI Kuhusu UTEKAJI & WASIOJULIKANA

Serikali katika kuimarisha masuala ya usalama na afya kazini

Power outages throughout Central Illinois

2 unusual aspects of SpaceX's IPO

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI

'USINITISHE MIMI, KILA MKENYA NI MKIKUYU' ~UHURU KENYATTA LAST WARNING TO RUTO

