MUSTAKBALI WA WAYAHUDI KWA MUJIBU WA QUR'AN TUKUFU - SHEIKH SULEIMAN KILEMILE - PART 1

Kwa karne nyingi watu hawa hawakuwa wakijulikana kama Wayahudi, bali walijulikana kama wana wa Israel (au wana wa Nabii Yakub) kama wanavyotajwa ndani ya Qur'an. Ni wale tu ambao walijitangazia utaratibu wa maisha unaofuata matakwa ya walimu wao wa Sheria, Mfumo ambao ndio wa Kiyahudi na wafuasi wake wakaitwa Wayahudi (yaani wafuasi wa dini ya Kiyahudi) Kabla ya ujio wa Nabii Isa (AS), Wayahudi waligawanyika makundi mawili. Kuna walioamua kuufuata utaratibu wa kuiheshimu Siku ya Sabato, amri iliyoachwa na Nabii Musa ndani ya Torati. Kundi hili ambalo ndilo kubwa likaitwa la Wasabian (Sabiin) ndani ya Qur'an. Na baada ya ujio Nabii Isa na kuondoka kwake, lilipatikana kundi jingine lililoitwa la Manasara (Wakristo) Lakini kuanzia karne ya 13, kwa ujumla walianza kuitwa Wayahudi kutokana na neno la Kirumi la Judea, lililomaanisha eneo walilopewa kukaa kabila moja la Yuda iliko Yerusalemu. Kabila hili miongoni mwa makabila 12, ndilo lililokuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa kujitawala kutoka kwa watawala wao Warumi. Hadi Mtume Muhammad (S.A.W) anahamia mjini Madina, tayari aliyakuta baadhi ya makabila ya Kiyahudi, yaliyokuwa yamelowea katika eneo hilo. Kuhamia kwa Wayahudi mjini Madina na sehemu nyingine za Waarabu kulitokana na sababu kadhaa na miongoni mwazo mbili ndizo huwa zinapewa umuhimu. Sababu ya kwanza, inasemekana kwamba Wayahudi walikuwa wanatarajia ujio wa Nabii mwingine atakayekuwa na nguvu ya kuwakomboa Wayahudi kutokana na kutawaliwa na Dola za kigeni, na kwamba kulikuwa na dalili katika maandiko yao, za Nabii yule kutokea katika nchi za Mashariki. Hivyo baadhi ya makabila ya Kiyahudi yalihamia mashariki katika ardhi za Waarabu wakidhani kuwa kama Nabii huyo atakapotokea basi atokee katika mojawapo ya kabila zile za kihamiaji. Sababu ya pili ni kwamba katika mwaka 70 AD, Jenerali wa Kirumi aliyeitwa Titus, alipigana na Wayahudi na kufanikiwa kuiteka Yerusalemu na hivyo kukomesha utawala wa Kiyahudi katika ardhi ya Wapalestina. Kufuatia hali hii wengi katika makabila ya Kiyahudi hawakupenda kutawaliwa wakihofia maisha yao, walikimbia na kuhamia katika nchi za Kiarabu na kuyakalia mabonde yenye rutuba kwa ajili ya kilimo na biashara. Kwa hatua hii wakawa walowezi katika nchi za Waarabu. Hadi mwanzoni mwa karne ya 7, makabila matatu ya Kiyahudi yalishaweka makazi yao mjini Madina, wakati ule ikiitwa Yathrib. Mji huu uliitwa Madina (Madinatun-Nabiy) baada ya ujio wa Mtume Muhammad (S.A.W) kwa heshima yake. Msuguano kati ya Waislam na Wayahudi, ulianza baada ya Mtume kuhamia Madina. Kadiri alivyoendelea kuwa maarufu na kukubalika kama Kiongozi wa umma, ndivyo ilivyozidi chuki ya baadhi ya Wayahudi dhidi yake. Kuna waliomkubali, na kuna wengine waliomkataa waziwazi na wengine kwa kujificha (wanafiki). Kwa kuwa Mtume alilenga katika kuijenga jamii yenye kufuata misingi ya amani, haki na usawa, Wayahudi walimuona kuwa ni tishio dhidi ya maslahi yao yaliyotokana na mufumo wao wa kinyonyaji. Pia kwa kuwa alikuwa ni Mtume, walikuwa wakimpinga na kuhojiana naye kutokana na kuzikosoa baadhi ya tafsiri za maandiko yao, wakisema hakuwa na maarifa juu ya mambo ya kiroho. Lakini kutokana na kushindwa kwao kuitoa kosa Qur'an, wengi wa Wayahudi wa Madina walimuona Muhammad kama Mtume wa kweli na kuamua kusilimu na kumfuata, licha ya wengine kuendeleza ubishi wao na mashaka. ......Sasa fuatana na Sheikh Suleiman Kilemile kutoka Tanzania, katika Mada hii inayowahusu Wayahudi...

MUSTAKBALI WA WAYAHUDI KWA MUJIBU WA QUR'AN TUKUFU - SHEIKH SULEIMAN KILEMILE - PART 2
▶︎

MUSTAKBALI WA WAYAHUDI KWA MUJIBU WA QUR'AN TUKUFU - SHEIKH SULEIMAN KILEMILE - PART 2

12 SURAH YUSUF (Tafsiri ya Quran kwa Kiswahili Kwa Sauti, Audio)
▶︎

12 SURAH YUSUF (Tafsiri ya Quran kwa Kiswahili Kwa Sauti, Audio)

SHEIKH KILEMILE-MWISHO WA MAISHA YA VIUMBE
▶︎

SHEIKH KILEMILE-MWISHO WA MAISHA YA VIUMBE

Ukweli juu ya Palestina | Shk. Stambuli Abdillahi Nassir
▶︎

Ukweli juu ya Palestina | Shk. Stambuli Abdillahi Nassir

AYA NA HEKAYA 02 | Sheikh Ali Asaa Ali Na Historia yake Katika Masomo Yake Mpaka Sasa
▶︎

AYA NA HEKAYA 02 | Sheikh Ali Asaa Ali Na Historia yake Katika Masomo Yake Mpaka Sasa

མཐོ་སློབ་འགྲིམ་བཞིན་པའི་བོད་རིགས་ན་གཞོན་དང་། ལྕོག་ལམ་གསར་གྱི་བརྒྱ་ཤོག་ལྔ་པའི་གཞིས་མི་སོགས་ལ་མཇལ་ཁ།
▶︎

མཐོ་སློབ་འགྲིམ་བཞིན་པའི་བོད་རིགས་ན་གཞོན་དང་། ལྕོག་ལམ་གསར་གྱི་བརྒྱ་ཤོག་ལྔ་པའི་གཞིས་མི་སོགས་ལ་མཇལ་ཁ།

Sheikh Amran Kilemile - Tafsiri Ya Quran Suratul Kahf Aya Ya 102 - 110
▶︎

Sheikh Amran Kilemile - Tafsiri Ya Quran Suratul Kahf Aya Ya 102 - 110

Uislam na amani ya Ulimwengu - Sheikh Suleiman Amran Kilemile
▶︎

Uislam na amani ya Ulimwengu - Sheikh Suleiman Amran Kilemile

Hili ni Tamko elekezi hukusu ARAFA. Sh. Kile mile.
▶︎

Hili ni Tamko elekezi hukusu ARAFA. Sh. Kile mile.

SHEIKH KILEMILE - UCHAGUZI MKUU NA AMANI YA TANZANIA
▶︎

SHEIKH KILEMILE - UCHAGUZI MKUU NA AMANI YA TANZANIA

Origins of Ashkenazi Jews (Ashkenazium Lectures Part 1)
▶︎

Origins of Ashkenazi Jews (Ashkenazium Lectures Part 1)

Umuhimu wa Subra katika Maisha ya Mwanadamu - Sheikh Kilemile
▶︎

Umuhimu wa Subra katika Maisha ya Mwanadamu - Sheikh Kilemile

Visiting the Muslim Island with over 8000 Mosques Lombok Indonesia 🇮🇩
▶︎

Visiting the Muslim Island with over 8000 Mosques Lombok Indonesia 🇮🇩

SAKATA LA SHEIKH WALID NA BELLA SHEIKH AFICHUA MSIYOYAJUA, MPANGO MBAYA ULIOANDALIWA, ADAI MAZITO
▶︎

SAKATA LA SHEIKH WALID NA BELLA SHEIKH AFICHUA MSIYOYAJUA, MPANGO MBAYA ULIOANDALIWA, ADAI MAZITO

Gary Wills, "What the Qur'an Meant: And Why It Matters"
▶︎

Gary Wills, "What the Qur'an Meant: And Why It Matters"

Ma amineysid meeshaan iney Somalia tahay, EYL. |You won't believe here is Somalia EYL.|
▶︎

Ma amineysid meeshaan iney Somalia tahay, EYL. |You won't believe here is Somalia EYL.|

Tafsiri Suratul Kahfi aya ya 99 SHEKHE KILEMILE
▶︎

Tafsiri Suratul Kahfi aya ya 99 SHEKHE KILEMILE

HUYU HATAKIWI KUWA SHEIKH:MZUNGUMZAJI SHEIKH KASSIM MAFUTA-ALLAH AMUHIFADHI
▶︎

HUYU HATAKIWI KUWA SHEIKH:MZUNGUMZAJI SHEIKH KASSIM MAFUTA-ALLAH AMUHIFADHI

Lengo la kuletwa Mitume na Vitabu- Sheikh Suleiman Kilemile - Part 1
▶︎

Lengo la kuletwa Mitume na Vitabu- Sheikh Suleiman Kilemile - Part 1

SHEIKH KILEMILE - MUONGOZO WA MTUME S.A.W KATIKA SIKU 10 ZA MWISHO WA RAMADHAN
▶︎

SHEIKH KILEMILE - MUONGOZO WA MTUME S.A.W KATIKA SIKU 10 ZA MWISHO WA RAMADHAN