PROF. BUSAGALA "WAKULIMA WA MPUNGA CHANGAMKIENI MBEGU YA SUPER BC/ TARI RICE ONE

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Prof. Lazaro Busagala amewasihi wakulima wa mpunga upande wa Zanzibar kuchangamkia mbegu ya Super BC ambapo kwa Tanzania Bara mbegu hiyo inaitwa TARI RICE ONE kwani mbegu hiyo ina tija kubwa kwa wakulima.