Nafasi ya Vijana katika kulinda na kudumisha amani ya nchi - Ubungo Manispaa

Matukio ya vurugu zilizotokea Oktoba 29 yamebaki kuwa kumbukumbu nzito kwa wakazi wengi wa Dar es Salaam, huku Ubungo ikiwa miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi kutokana na vurugu hizo zilizosababisha hasara za mali na kugharimu maisha ya wananchi. Je, vijana wanawezaje kuwa sehemu ya suluhisho badala ya kuwa sehemu ya vurugu? Katika makala hii, tunaangazia nafasi ya vijana katika kuhakikisha matukio kama hayo hayajirudii tena.