ANDAA MIEMBE YA KISASA MWENYEWE HAPO NYUMBANI KWAKO INAYOZAA NDANI YA MIAKA2.

Chakuzingatia ni kutafuta embe lililoiva,chomoa kokwa lake,kisha lichunguze kama halina ugonjwa,halafu lipande kwenye kiriba,naada ya mche kuota na kufikia urefu wa wastani wa rula,tafuta tawi la mwembe ambao umeshakomaa,na tayari unazaa maembe makubwa na matamu,kisha kata kichwa cha ule mche wako,chonga tawi lako,kisha pasua huo mche na chomeka lile tawi lako,halafu funga kwa kamba ya plastiki,na funika kwa mfuko wa plastiki ili kuzuia upepo usikaushe,halafu weka mche wako kivulini na mwagilia mara3kwasiku.