Wimbo huu ukakuinue ukakufanye ujue thamani ya Neema na Rehema ya Kristo kwenye maisha yako Amen.

Nadharia ya wokovu ipo wazi sana, Tumeokolewa kwa neema kwa njia ya imani iliyo katika Kristo Yesu. Kituo kikuu! Wokovu huo Paulo anaita ni injili ya neema ya Mungu (Waefeso 3:2); Injili ya Mungu (Warumi1:1). Anayeainisha wokovu wa mwamini ni Mungu sio watu wala shetani au hata dhambi za watu. Alichofanya Mungu katika Kristo ni cha milele, hakipotei baada ya mtu kukosea hata kuwa katika hali ya matendo ya mwili. Kwa watu wa dini wokovu bado ni fumbo kubwa, wanafikiri mtu anaweza kupoteza wokovu baada ya kuzaliwa mara ya pili. Ni kama mtoto anapozaliwa ni kitu gani akifanya ambacho ni kibaya kitamfanya asiwe mtoto au asizaliwe tena? Unagundua hakuna majibu! Badala yake dini inabaki kutuhumu Neema ya Mungu kwamba ni kutoa leseni ya kutenda dhambi. Labda huko kutenda dhambi kama wanakuwa hawamaanishi matendo ya mwili, kwani matendo ya mwili ni kwa yoyote (wakiwemo watu wa dini, wapagani, waamini) asiyejitiisha katika maarifa ya neema ya Mungu kuhusu Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo. COVENANT GRACE CHURCH