KILIMO CHA NYANYA:Semina kubwa ya kilimo cha nyanya (IMARA F1) iliyoendeshwa na East West Seeds
Imara F1 nyanya bora ya chotara yenye mavuno mengi inayofaa wakati wa mvua na kiangazi. Mbegu bora za nyanya Kutokana na tabia ya ukuaji, mbegu za nyanya zinagawanyika katika makundi mawili: 1. Nyanya ndefu (indeterminate) kwa mfano ANNA F1, Tengeru 97, Marglobe (M2009). Aina hizi za nyanya hufanya vizuri zaidi zinapopandwa ndani ya greenhouse. Uvunaji wake ni wa muda mrefu; zipo ambazo zinavunwa hata zaidi ya miezi 6, yaani hiyo miezi 6 ni ya uvunaji. 2. Nyanya fupi (determinate) kwa mfano Tanya,Imara F1, Cal J, Mwanga, Onyx, Roma VF (nyanya mshumaa) Kulingana na uchavushaji, nyanya zinagawanyika katika makundi mawili: 1. Nyanya za OPV (Open Pollinated Variety) – Hizi ni aina za kawaida 2. Nyanya Chotara – hybrid: Hizi ni nyanya zilizoboreshwa, aina hii zina mavuno mengi, kati ya hizo zipo aina fupi na ndefu. mtaji wa kilimo cha nyanya gharama za kilimo cha nyanya utajiri wa kilimo cha nyanya kilimo cha nyanya kiangazi pdf kilimo cha nyanya wakati wa mvua kilimo cha nyanya 2020 kilimo cha nyanya ndefu kilimo cha nyanya masika Jinsi ya kupanda nyanya • Weka samadi viganja viwili au gram 5 za mbolea ya kupandia kwenye shimo kabla ya kupanda mche. • Hamisha miche toka kitaluni pamoja na udongo wake • Sambaza mizizi vizuri kwenye shimo bila kukunja. • Fukia miche kina kile kile ambacho shina lilikuwa limefukiwa kitaluni. • Mwagilia maji ya kutosha kulingana na unyevunyevu uliopo kwenye udongo kisha weka matandazo na kivuli ili kupunguza uharibifu unaosababishwa na mionzi ya jua. Jinsi ya kutunza nyanya shambani Umwagiliaji wa nyanya Nyanya, kama ilivyo kwa mazao mengine, zinahitaji maji mengi ili kuzaa matunda yenye afya. Kutegemeana na aina ya udongo, unaweza kumwagilia nyanya mara mbili kwa wiki. Hakikisha unapanga ratiba maalum ya kumwagilia na unaifuata ili kuepuka kumwagilia kiholela holela kwani umwagiliaji usio na mpangilio huathiri afya ya matunda ya nyanya na kupelekea nyanya kuoza kitako (tomato blossom end rot). Unapotumia vifaa kama water can au mpira jitahidi sana usimwagilie kwenye majani ya mmea au matunda kwa sababu kulowesha mmea kunavutia wadudu na magonjwa ya ukungu unaoharibu nyanya. Zingatia: usituamishe maji kwenye bustani au shamba la nyanya. Palizi: Kudhibiti magugu Hakikisha shamba ni safi wakati wote, palilia shamba na hakikisha magugu yote hasa yale ya jamii ya nyanya yamelimiwa chini. Palilia shamba lako wiki ya pili au ya tatu baada ya kupandikiza miche, lakini unaweza kupalilia kila unapoona magugu kwani shamba linatakiwa kuwa safi muda wote. Unaweza kuondoa magugu kwa kutumia dawa za kuua magugu au jembe la mkono. Magugu ni hatari kwa sababu tatu: Kwanza: magugu yanashindana na mimea katika kuchukua nafasi na hivyo mimea kushindwa kujitanua. Pili: magugu huzuia mimea ya nyanya kupata mwanga wa jua wakutosha hivyo kuifanya mimea kushindwa kujitengenezea chakula cha kutosha. Na tatu: magugu hushindana na mimea ya nyanya kufyonza virutubisho/chakula ardhini kitu ambacho kinapelekea mimea kuwa dhaifu. Pia magugu yanahifadhi wadudu na magonjwa na hivyo kuhatarisha zaidi usalama wa nyanya. Mahitaji ya mbolea kwenye nyanya Mbolea za kupandia nyanya Tumia mbolea ya DAP au Minjingu wakati wa kupandikiza miche shambani. Kiasi cha gram 5 ambayo ni sawa sawa na kifuniko kimoja cha soda inatosha kwa kila shimo lenye mche mmoja. Tanguliza mbolea kwanza kwenye shimo kisha funika na udongo kiasi ili mbolea isigusane moja kwa moja na mizizi ya nyanya. Mbolea za kukuzia nyanya Tumia mbolea kama vile CAN, NPK, au SA kukuzia mimea ya nyanya. Mbolea ya kukuzia iwekwe kipindi cha wiki mbili au tatu baada ya kupandikiza nyanya shambani. Tumia kifuniko kimoja cha soda kwa shina. Mbolea hii iwekwe kuzunguka shina la nyanya kwa umbali wa sentimeta 5 kutoka kwenye shina. Mbolea hii inaweza kuwekwa mara mbili kabla ya mvuno wa kwanza. Ili kurefusha kupindi cha uzaaji wa zao la nyanya (na hata mazao mengine yatoayo matunda kama vile nyanya chungu, biringanya, na pilipili hoho) inapaswa kuongezea mbolea katika kipindi cha uvunaji mfano baada ya kuvuna mara mbili unashauriwa kuongeza mbolea ya samadi na mbolea kama vile NPK. Kupogolea majani Kupunguza majani ni muhimu pia katika kupunguza maambukizo ya ukungu katika shina na pia kutoa nafasi ili mwanga kupenya na kuruhusu mzunguko wa hewa. Kwa nyanya ndefu, majani ya chini ya matunda huondolewa kadiri unavyo endelea kuvuna. Kusimikia miti (staking) Nyanya ziwekewe miti/mambo ili kuzuia zisianguke au kutambaa kwenye udongo, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara mengi kwa nyanya. Nyanya zinazotambaa zinahitaji kusaidiwa kuonyeshwa njia ili zisiguse chini. #mkulimasmart #shambadarasa

#TBC1:SHAMBANI:KESHO BORA | MAFANIKIO YA KILIMO CHA NYANYA KATIKA MATUMIZI YA MBEGU BORA

MRISHO MPOTO NDANI YA KILIMO CHA NYANYA

FORI Yafunga Pazia la miaka mitatu ,ikiacha Urithi wa Maarifa,Ustahimilivu na mafanikio Mashambani.

JE! NI MIEZI IPI YA KUPANDA NYANYA ILI UKUTANE NA PESA?

#TBC: SHAMBANI KESHO BORA-KILIMO CHA NYANYA KATIKA MSIMU WA MVUA.

MBEGU YA KITUNGUU RED PLANET F1, MWEZI MMOJA BAADA YA KUVUNWA, INAFAA KUHIFADHIKA MUDA MREFU

MBUNGE WA KATAVI AVUNA PESA BUNGENI BAADA YA KUGONGA NONDO ZITO JUU YA UVUNJIFU WA MAADILI.

BALAA LA DHAHABU F1 MBEGU YA NYANYA 🍅/ MKULIMA ATOA USHUHUDA

KAA HAPA SE02 EP07 FULL SHOW | MTAALAMU WA KILIMO | EAST-WEST SEED TANZANIA | DANIEL KABAKA

How We Grow Sweet Corn from Start to Finish (and the $ per acre)

MRISHO MPOTO AVUNA NYANYA ZA MAMILIONI "NILIANZA KWA HASARA YA MILIONI 60"

Growing Tomatoes in Bottles on Balcony for Fresh Fruit All Year

KILIMO CHA NYANYA KINAMKOMBOA MKULIMA // KILIMO SOKONI

Never Buy a Water Pump Again! A 65-Year-Old Plumber Made His Own Water Pump Using PVC Pipes | Update

ZIFAHAMU AINA ZA MBOLEA NA MATUMIZI YAKE SAHII / KUKUZIA NA KUPANDIA

KANTANGAZE UGONJWA WA NYANYA UNAODHIBITIWA NA MBEGU CHOTARA ZA IMARA

BALAA LA MRISHO MPOTO AINGIZA MILIONI 20 NDANI YA MIEZI MITATU, ATAJA SIRI..

MKULIMA NAMBA MOJA MKOA WA DSM UYU HAPA KUTOKEA KIGAMBONI

Why Single-Origin Coffee Is So Expensive | So Expensive | Business Insider

