NGUVU MAOMBI KATIKA KUHAMISHA MILIMA - ROLF KIBAJA - PRT 6

Somo hili tunajifunza Kusuhu umuhimu wa Maombi katika kuhamisha milima ambayo inaweza ikawa ni Changamoto mbalimbali mtu anazo zipitia. Tunahitaji kuwa na Ushirika na Mungu kupitia maombi ili zile changamoto ziondoke na kuhamishwa. Marko 11:23-24 inasema, 23 Amin, nawaambia, yeyote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. 24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.