KESI YA IDRIS SULTAN: MASHAHIDI 15 KUSIMAMA KIZIMBANI, ASOMEWA MAELEZO YA AWALI
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga Agosti 5, mwaka huu kuanza kusikiliza jumla ya mashahidi 15 katika kesi inayomkabili msanii Idris Sultan ya kushindwa kusajili laini ya simu iliyokuwa inamilikiwa na mtu mwingine. Mbali ya Idris, mshitakiwa mwingine ni Innocent Maiga. Wakili wa Serikali, Sylvia Mitanto amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rashid Chaungu kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ambapo alianza kwa kumsomea upya mashitaka yanayomkabili. Amedai kati ya Desemba 1, 2019 na Mei 19, 2020 katika eneo la Mbezi Beach, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Idriss alitenda kosa la kushindwa kufanya usajili wa laini ya simu inayotumiwa na mtu mwingine. Inadaiwa katika kosa hilo mshitakiwa alitumia kadi ya simu iliyomilikiwa na Innocent Maiga bila kuripoti kwa mtoa leseni. Katika shitaka jingine linamkabili mshitakiwa Maiga ambapo anadaiwa kutenda kosa la kushindwa kutoa taarifa ya mabadiliko ya kadi ya simu kutoka kwake kwenda kwa Idriss kosa analodaiwa kulitenda kati ya Desemba 1, 2019 na Mei 19, mwaka huu eneo la Mbezi Beach Kinondoni jijini Dar es Salaam. Pia inadaiwa Mei 5, mwaka huu Mkuu wa Upelelezi Kinondoni alipewa taarifa kwamba Idriss anatumia kadi ya simu ya Vodacom ambayo haijasajiliwa kwa jina lake na kwamba alitakiwa kuripoti Kituo cha Polisi Oysterbay ambapo alifanya hivyo. Ilidaiwa Polisi walienda kufanya upekuzi nyumbani kwa Idriss na kubaini uwepo wa laini hiyo ya simu na kwamba alikuwa akiitumia kwa mawasiliano yake ya kila siku licha ya kusajiliwa kwa jina la Maiga. Inadaiwa Idriss alikiri kutumia kadi hiyo ya simu ambayo ilikuwa ikimilikiwa kabla na Maiga na kwamba alikiri kuitumia tangu Desemba mwaka jana. Mshitakiwa Maiga anadaiwa kukiri kumiliki kadi hiyo na alimpatia Idriss aweze kuitumia na kwamba alikiri kutoripoti kwenye mamlaka kuhusu mabadiliko ya kadi hiyo. Hata hivyo, washitakiwa hao ambao wanawakilishwa na Wakili Jebra Kambole na Maria Mushi, walikiri maelezo yao binafsi pamoja na mashitaka yanayowakabili mahakamani hapo na kukana maelezo ya mashitaka. Upande wa mashitaka umedai wataleta mashahidi 15 na kama watahitaji kuongeza au kupunguza mashahidi wataieleza mahakama na kwamba wataeleza idadi ya vielelezo watakavyokuwa navyo kesi itakapoendelea.

#PAROKIA YA SWASWA: ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU SHEREHE YA MWILI NA DAMU YA BWANA WETU YESU KRISTO

How To Capture Your Morning Angel

Ghetto Kids Bruno's First Golden Buzzer Full Performance | Britain's Got Talent 2023 Auditions WK 1

Mascha und der Bär 🍭 Süßes Leben🍭 Episodensammlung 👧🐻 Masha and the Bear 2022

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds

MSIGWA AFUNGUKA YOTE: Kilichomuondoa CCM / CHADEMA ALIYOIACHA vs ALIYORUDI

WANAHARAKATI : KUREJEA KWA HALIMA MDEE CHADEMA GODBLESS LEMA KIKANGOONI,MBINU MPYA MAANDAMANO TAR 7
![MLINZI Full Episode [ 5 ] #love](https://i.ytimg.com/vi/nqs9-MZtx8w/hqdefault.jpg?sqp=-oaymwEnCNACELwBSFryq4qpAxkIARUAAAAAGAElAADIQj0AgKJDeAG4AvMY&rs=AOn4CLBxwj-TyLA4BUgXbHja-_-SlVvoAw&usqp=CCY)
MLINZI Full Episode [ 5 ] #love

周恩来怎么死的?真正原因,没人敢说!

Ego Bodybuilder HUMILIATED Beyond Belief 🤯 | Anatoly GYM PRANK

Rais Samia wa Tanzania anatafuta nini Urusi? Katika Dira ya Dunia TV

SHAMBA LA MFANO KWA WAFUGAJI MZEE SHAMBA KUBWA LONGIDO KISIMA CHA MAARIFA YA MIFUGO

FAITH STORY

I have never eaten such delicious zucchini! Nobody knows this recipe! Only 2 ingredients!

My Golden Retriever Heals a Terrified Rescue Kitten in Just 3 Meetings!

Dieser 5-Jährige SINGT Französisch ✨🎤 Und alle flippen aus! 🎶 I Staffel 9 I Das Supertalent

Kuomba nı jambo la msıngı

Bunge la ulaya lapiga kura ya mwisho kuzuia misaada na ufadhili kwa Tanzania Wakili garubindi aibuka

I’m NOT Frying Eggplant Anymore — Few Know This Trick! A Restaurant-Style Eggplant Recipe for Dinner

