JEMEDARI | 1ST ALBUM (2019) | FURAHINI KWAYA FPCT MPANDA | HD
Maneno ya wimbo huu yanapatikana 2 Wafalme 5:1-25 NEN Wakati huu, Naamani alikuwa jemadari wa jeshi la mfalme wa Aramu. Alikuwa mtu mkuu mbele ya bwana wake na aliyeheshimiwa sana, kwa sababu kupitia kwake, BWANA alikuwa amewapa Aramu ushindi. Alikuwa askari hodari, lakini alikuwa na ukoma. Siku hizo vikosi kutoka Aramu vilikuwa vimeenda na vikawa vimemteka msichana kutoka Israeli, naye akamtumikia mkewe Naamani. Akamwambia bibi yake, “Kama bwana wangu angemwona nabii aliye huko Samaria! Angemponya ukoma wake.” Naamani akaenda kwa bwana wake na kumwambia alichosema yule msichana kutoka Israeli. Mfalme wa Aramu akamjibu, “Hakika, nenda. Nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaondoka, akiwa amechukua talanta kumi za fedha, shekeli elfu sita za dhahabu, na mavazi kumi. Barua aliyopelekea mfalme wa Israeli iliandikwa hivi: “Pamoja na barua hii ninamtuma mtumishi wangu, Naamani, kwako ili uweze kumponya ukoma wake.” Mara mfalme wa Israeli alipomaliza kuisoma ile barua, akararua mavazi yake na kusema, “Je, mimi ni Mungu? Je, mimi naweza kuua na kufufua tena? Kwa nini huyu mtu anamtuma mtu ili mimi nipate kumponya ukoma wake? Tazama jinsi anavyotafuta kuanzisha ugomvi nami!” Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alikuwa amerarua mavazi yake, akamtumia ujumbe huu: “Kwa nini umerarua mavazi yako? Mwamuru mtu huyo aje kwangu, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaenda, akiwa na farasi wake na magari yake ya vita, na kusimama mlangoni mwa nyumba ya Elisha. Elisha akamtuma mjumbe kumwambia, “Nenda uoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itapona, nawe utatakasika.” Lakini Naamani akaondoka akiwa amekasirika, akasema, “Hakika nilidhani kwamba angetoka nje, asimame na kuliitia jina la BWANA Mungu wake, na kupitisha mkono wake juu ya mahali penye ugonjwa ili aniponye ukoma wangu. Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora kuliko mito yoyote ya Israeli? Je, nisingeweza kuoga ndani ya hiyo mito na kutakasika?” Basi akageuka na kuondoka kwa hasira kuu. Watumishi wa Naamani wakamwendea na kumwambia, “Baba yangu, kama huyo nabii angekuambia kufanya jambo lililo kubwa, je, hungelifanya? Je, si zaidi sana basi, anapokuambia, ‘Oga na utakasike!’ ” Hivyo akashuka na kujizamisha ndani ya Yordani mara saba, kama vile huyo mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia, nayo nyama ya mwili wake ikapona na kutakasika kama ya mwili wa mvulana mdogo. Kisha Naamani na wahudumu wake wote wakarudi kwa yule mtu wa Mungu. Akasimama mbele yake na kusema, “Sasa najua kwamba hakuna Mungu katika ulimwengu wote isipokuwa katika Israeli. Tafadhali sasa upokee zawadi kutoka kwa mtumishi wako.” Nabii akajibu, “Hakika kama BWANA aishivyo, ninayemtumikia, sitapokea kitu hata kimoja.” Ingawa Naamani alimsihi sana, yeye alikataa. Naamani akasema, “Ikiwa hutapokea, tafadhali mtumishi wako na apewe udongo kiasi cha mzigo wa kuweza kubebwa na punda wawili, kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa na dhabihu kwa mungu mwingine isipokuwa BWANA.

Furahini Choir ACT Kichangani Mpanda - Atakujia (Official Video)

Katoro a kwaya Kampeni

SISI ILEWE | 2026 Latest Nigeria Movie - Ego Nwosu, Kunle Remi, Kamo State

"The Fall of Megachurches: Why Joel Osteen's Lakewood Church is Collapsing"

DAUDI | 1ST ALBUM (2019) | FURAHINI KWAYA FPCT MPANDA | HD

DALILI ZA KURUDI KWA YESU ( 02 ) Rabbi Abshalom Longan •RUNZEWE GEITA

AIC Nyankumbu Vijana Choir (NVC) - MASHUHURI

WIMBO - NI NEEMA(Official Video). UPENDO KWAYA - EAGT-KIWIRA Mbeya TZ

Powerful Quran Recitation for Night | Ayatul Kursi, Yasin, Alkahfi, AlWaqiah, AlMulk by Alaa Aqel

NJIA MOJA CHOIR - APANDAE KWA MWILI (OFFICIAL VIDEO)

3 AMENIBADILISHA(LEGION) BY FURAHINI KWAYA F.P.C.T MPANDA

8 June 2026

Tiyamike - Chanyumbu CCAP Chisomo Women Choir

BWANA YESU ANASEMA | 1ST ALBUM (2019) | FURAHINI KWAYA FPCT MPANDA | HD

Yeshua: 3 Hour Prayer, Meditation & Soaking Worship with Scriptures & Nature 🌿CHRISTIAN piano

CHAKULA HUU WIMBO MZURI SANA

I Will Not Give Up 🙏🏾 Deep Gospel Blues Prayer | Emotional Testimony Song | Grace Gospel Blues
![🔴#MWAMPOSALIVE [14.06.2026] IBADA YA MAOMBI , MAOMBEZI NA KUFUNGULIWA](https://i.ytimg.com/vi/wudYJiw_iVA/hqdefault.jpg?sqp=-oaymwEjCNACELwBSFryq4qpAxUIARUAAAAAGAElAADIQj0AgKJDeAE=&rs=AOn4CLCJ2Eep8cyp-b12WeurbQz710jrQQ)
🔴#MWAMPOSALIVE [14.06.2026] IBADA YA MAOMBI , MAOMBEZI NA KUFUNGULIWA

Jina la Yesu - Mama Mchungaji Lawi

