ROZARI YA MATESO SABA YA MAMA BIKIRA MARIA | SEVEN SORROWS OF VIRGIN MARY
ROSARI YA MACHUNGU SABA YA BIKIRA MARIA Kwa jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina Sala ya kwanza Ee Mungu wangu, nakutolea Rosali hii ya machungu saba ya Bikira Maria kwa ajili ya utukufu wako na kwa heshima ya mama yako Mtakatifu sana. Nitawaza na kushikania naye katika haya aliyopata. Nawe Maria Mama yetu nakuomba, kwa heshima ya machozi uliyomwaga wakati ulipopatwa na machungu haya, utujalie kutubu dhambi zetu. Amina. Salamu Maria X 3 Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA KWANZA (LK 2:25-35) Katika uchungu wa kwanza tunakumbuka wakati mzee mtakatifu Simeoni alipomtabiria Maria kwamba upanga wa uchungu utaufuma moyo wake, akimaanisha mateso na kufa kwake Yesu Kristo mwanae. Tuombe neema ya kuvumilia mateso. Baba Yetu x 1 Salamu Maria x 7 Atukuzwe Baba, Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA PILI (MT 2:12-18) Katika uchungu wa pili tunakumbuka wakati Maria alipolazimika kukimbilia Misri kwasababu Herode katili alitaka kumuua mtoto Yesu. Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu. Baba Yetu x1 Salamu Maria x7 Atukuzwe Baba, Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA TATU (LK 2:41-51) Katika uchungu wa tatu tunakumbuka wakati Maria alipompotezs mwanae mpendwa na kwa siku tatu akamtafuta kwa uchungu mpevu na machozi. Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu. Baba Yetu x 1 Salamu Maria x7 Atukuzwe Baba Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA NNE (LK 23:26-31) Katika uchungu wa nne tunakumbuka wakati Maria alipokutana na mwanae wa pekee akiwa amebeba msalaba akielekea mlima Kalvari ambako alikua akienda kusulubiwa kwa ajili ya wokovu wetu. Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote. Baba Yetu x1. Salamu Maria, x7 Atukuzwe Baba, Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA TANO (YOHN 19:25-27) Katika uchungu wa tano tunakumbuka wakati Maria alipomwona mwanae Yesu ametundikwa juu ya msalaba na damu nyingi ikimwagika kutoka sehemu zote wa mwili wake. Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria. Baba Yetu x1 Salamu Maria, x7 Atukuzwe Baba, Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA SITA (YHN 19:38-40) Katika uchungu wa sita tunakumbuka wakati Maria alipomwona askari akimchoma mwanae ubavuni kwa mkuki na wakati mwili wa Yesu, baada ya kusgushwa msalabani, ulipolazwa mikononi mwake. Tuombe neema ya kutotenda dhambi. Baba Yetu x1 Salamu Maria, x7 Atukuzwe Baba, Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. UCHUNGU WA SABA (THN 19:40-41) Katika uchungu wa saba tunakumbuka wakati Maria alipoona mwili wa mwanae wa pekee Yesu ukizikwa kaburini akitengana na mwanae ambaye kweli alimpenda mno. Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria. Baba Yetu x1. Salamu Maria, x7 Atukuzwe Baba, Ee Bikira Maria, Mama mwenye huruma, tukumbushe kila wakati mateso ya Yesu Kristo mwanao. TUOMBE: Ee Bwana Mungu wetu, kwa njia ya mateso na kifo cha Mwokozi wetu Yesu Kristu na kwa masumbuko yaliyompata mama yake Bikira Maria, ulileta wokovu kwetu sisi wakosefu. Twakuomba utujalie huu wokovu, tupate kuacha njia za dhambi na kupata yote mema aliyotuahidia Yesu Kristo yeye anayeishi na kutawala nawe na Roho Mtakatifu sasa na milele. Amina. KUMBUKA Kumbuka , Ee Bikira Maria, mwenye rehema, haijasikilika kamwe kwamba ulimwacha mtu aliyekimbilia ulinzi wako, akiomba msaada wako, akitaka umuombee. Nami kwa matumaini hayo ninakukimbilia ee Mama Bikira mkuu wa Mabikira, ninakuja kwako, ninasimama mbele yako nikilalamika mimi mkosefu, Ee Mama wa Neno la Mungu, usikatae Maneno yangu, bali uyasikilize kwa wema na unitimizie. Amina.

Kwa Ajili Ya Mateso Makali Ya Yesu

๐๐๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐ ๐ ๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐๐๐ ๐(๐๐ฎ๐ฆ๐๐ญ๐๐ง๐จ ๐ง๐ ๐๐ฎ๐ฆ๐๐ฉ๐ข๐ฅ๐ข)

Rozari Matendo ya Mwanga. Rozari ya Alhamisi.

ROZARI YA MACHUNGU SABA YA BIKIRA MARIA | LITANIA YA MAMA WA MATESO| SEVEN SORROWS OF VIRGIN MARY

FATIMA: 3 tajne, ฤudo Sunca i ลกto znamo o ukazanjima

SIKU YA KWANZA | NOVENA KWA MTAKATIFU RITA WA KASHIA

๐Mary, Undoer of Knots โ Powerful Prayer for Urgent Help and Open Paths

ROZARI YA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

๐ด NOVENA KWA MTAKATIFU RITA WA KASHIA - SIKU 12

NYIMBO ZA KUABUDU NA MAOMBI | WORSHIP & PRAYER SESSION ๐ฅYAWEZEKANA TV

Sala ya Rozari Takatifu ya Huruma ya Mungu

ROZARI YA DAMU AZIZI YA YESU KRISTO (1) // Valeriana Simon

NYIMBO ZA MAMA BIKIRA MARIA | BIKIRA MARIA SONGS MIX

Divine Mercy Chaplet audio Swahili with lyrics

๐๐จ๐ณ๐๐ซ๐ข ๐๐๐ค๐๐ญ๐ข๐๐ฎ( ๐๐๐ญ๐๐ง๐๐จ ๐ฒ๐ ๐๐๐ก๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ-๐๐ฎ๐ฆ๐๐ง๐ง๐ ๐ง๐ ๐๐ฃ๐ฎ๐ฆ๐๐)

Tusali Rozari ya Huruma ya Mungu na Litania ya Huruma ya Mungu || Valeriana Simon

FAHAMU NGUVU YA MAOMBI USIKU WA MANANE.

Zaburi Swahili | Good News | Audio Bible

Pray This Prayer ONCE with Virgin Mary & Saint Anthony for an URGENT Miracle Today ๐

