NENO LA SIKU | Yohana 5 | Maombi Ya Kushinda Dhambi Inayokutesa | Isaac Javan

Leo tunasoma kitabu cha Yohana sura ya tano, na tunaenda kufanya maombi ya kushinda dhambi inayokutesa. Dhambi ni mlango unaotumika kupitisha vifungo vya kiroho. Na dhambi ni sababu inayompa shetani uhalali wa kutesa maisha ya watu. Katika maombi ya leo, YESU anaenda kutupa nguvu na uweza wa kushinda dhambi, na kutuwezesha kuishi maisha matakatifu yanayompendeza Mungu. Tunapofanikiwa kushinda dhambi, shetani anapoteza uhalali wa kututesa na kutufunga kwa vifungo vya kiroho. Nami nakuombea ushindi mkuu siku ya leo. BWANA akuonekanie na akuweke huru wa utukufu wa jina lake. Ameen! Isaac Javan +255 745 76 45 72