DIVA AFICHUA MAZITO YA WASAFI NA JUMA LOKOLE,NILIPENI MSHAHARA WANGU,AALIYA KAOMBA KAZI CROWN FM

#diva #wasafifm #jumalokole #dida VITA YA MANENO YA DIVA MALINZI NA JUMA LOKOLE YAINGIA AWAMU MPYA! “TUNAENDA BAMPA TO BAMPA!” Sakata la maneno kati ya Diva Malinzi na Juma Lokole linaendelea kushika kasi mitandaoni huku kila upande ukiendelea kurushiana vijembe na tuhuma nzito. Yote yalianza baada ya Diva Malinzi kufunguka kuhusu Marehemu Dida na kudai kuwa alimpenda sana na kumchukulia kama dada yake, lakini baadaye aligundua kuwa baadhi ya mambo aliyokuwa akimweleza kwa siri yalikuwa yakitumiwa vibaya. “Nilikuwa nampenda sana Dida na sijawahi kumkosea. Kwangu alikuwa kama dada. Muda mwingi nilimshirikisha mambo yangu ya siri na alikuwa akinipa ushauri. Ila alikuwa nyoka na nilitambua baada ya kufa kwake,” alisema Diva. Kauli hiyo ilizua mjadala mkubwa mtandaoni na kumfanya Juma Lokole kuingia kati kwa maneno makali akimshutumu Diva kwa kusubiri hadi baada ya kifo cha Dida ndipo aseme hayo. “Tena mnafiki haswa! Mbona kangoja afe ndiyo aseme? Sasa tutamsemea yeye. Si hodari wa kiki? Wacha twende kiki kwa kiki. Simpendi mimi huyu dada, Mungu anisamehe,” aliandika Juma Lokole. Baada ya maneno hayo kusambaa, Diva naye aliamua kuvunja ukimya na kujibu kwa hasira huku akidai kuwa amekuwa akivumilia mashambulizi ya maneno kwa miaka mingi. “Yaani sina unyonge huo tena. Tutaenda bampa to bampa. Nashangaa sana kwanini baadhi ya watangazaji wanaruhusiwa kutumia redio na televisheni kuwashambulia watu. Kama mnamwaga mboga, mimi nitamwaga ugali.” Diva alisema kwa miaka mitano amekuwa akizungumziwa vibaya, kutukanwa na kushambuliwa kwa maneno lakini amekuwa akichagua kukaa kimya kwa ajili ya kuheshimu sehemu aliyokuwa akifanya kazi. “Nimeongelewa vibaya kwa miaka 5 mizima. Nimevumilia sana. Sasa niko huru. Mtu yeyote atakayenivaa sitakaa kimya. Sitakubali kugeuzwa content ya watu.” Katika ujumbe wake, Diva pia alieleza kuwa kuondoka kwake kazini hakukutokana na kushinikizwa bali ilikuwa ni maamuzi yake mwenyewe baada ya kuchoshwa na mazingira ya migogoro na mashambulizi ya mara kwa mara. “Niliondoka mwenyewe. Nilichagua amani yangu. Nimeamua kufanya podcast zangu, biashara zangu na kutengeneza hela zangu. Sina tatizo na mtu yeyote.” Lakini mambo hayakuishia hapo. Baada ya Juma Lokole kuandika kuwa Watanzania walifurahia kuondoka kwa Diva na kumtaka aache kumtaja Marehemu Dida, Diva alirejea tena kwa ujumbe mwingine mrefu zaidi uliokuwa na mashambulizi ya moja kwa moja kwa Juma. “Mmefurahi kuondoka? Aliyewaambia nilikuwa nataka kukaa nani? Nimeamua mwenyewe. Mbona wengine wameondoka na hamjawashambulia? Kwa nini ni mimi pekee?” Diva alisema maisha yake hayajawahi kutegemea ajira pekee kwani hata kabla ya kuondoka alikuwa akiendesha biashara zake binafsi zilizokuwa zikimwingizia kipato. “Tangu mwaka jana nilikuwa nalipa bills zangu kwa biashara zangu. Nilikuwa naishi vizuri kabisa. Nina talent na ninaweza kwenda popote. Leo niende BBC, kesho niende sehemu yoyote duniani. Hilo si jambo linalowahusu.” Katika moja ya sehemu zilizovuta hisia za wengi, Diva alimjibu Juma kuhusu kumuita “ajuza” huku akidai kuwa Juma ni mkubwa wake kwa umri. “Unaniita ajuza wakati umezeeka kuliko mimi. Hicho ndicho kinachonichekesha. Kati yangu na wewe nani hasa ni kituko?” Diva pia aliwashambulia wale wanaomuunga mkono Juma akisema wengi wao ni watu wanaofurahia kuona wengine wakidhalilishwa. “Wanaokusapoti ni hao bullies wenzako. Lakini hiyo hainishtui hata kidogo.” Akionyesha wazi kuwa hana mpango wa kurudi nyuma, Diva alisema safari hii hatakaa kimya kama alivyofanya miaka iliyopita. “Watch me. Unyonge huo sina tena. Imetosha. Sitakaa tena niwe content ya watu huku nikiwa kimya.” Katika madai mazito zaidi, Diva alisema ana ujumbe na taarifa nyingi zinazoweza kubadilisha simulizi za baadhi ya watu wanaojifanya kumchukia hadharani. “Nina simu na message nyingi sana. Watu unaosema walifurahia kuondoka kwangu walikuwa wananiomba hata nauli. Wapo wanaolalamikia maisha yao na malipo yao. Mkinitafuta sana nitafungua kila kitu.” Aidha, Diva alidai kuwa watu wengi wanajua ukweli lakini wanaamua kukaa kimya kwa sababu zao binafsi. “Mnadhani kila mtu ni chawa? Watu wana taaluma zao na wana maumivu yao makubwa. Jiheshimuni.” Akimalizia ujumbe wake, Diva alisema kuwa kama kuna watu waliamua kumdhalilisha hadharani basi naye yupo tayari kujibu hadharani. “Kama mliamua kunidhalilisha basi tutadhalilishana. Sitakaa kimya tena. Never ever again.” Mpaka sasa Juma Lokole bado hajajibu kauli hizo za mwisho za Diva, jambo ambalo limewaacha mashabiki wakingojea kuona nani atatoa kauli nyingine katika vita hii ya maneno ambayo inaonekana ndiyo kwanza imeanza. je, katika sakata hili unaona nani ana hoja zaidi kati ya Diva Malinzi na Juma Lokole? Je, Diva ana haki ya kujibu baada ya miaka ya ukimya au alipaswa kupuuza yote? Maoni yako ni yapi?

Juma Lokole afunguka Diamond kumfukuza Diva kazi Wasafi Media| Hakuna anayemtaka| Hasara kubwa sana
▶︎

Juma Lokole afunguka Diamond kumfukuza Diva kazi Wasafi Media| Hakuna anayemtaka| Hasara kubwa sana

WOLPER: KAULI YA KAJALA ILINISHANGAZA KAMA HARMONIZE ALIKUWA ANATUCHANGANYA
▶︎

WOLPER: KAULI YA KAJALA ILINISHANGAZA KAMA HARMONIZE ALIKUWA ANATUCHANGANYA

//የሻይ ሰአት// "እንደ ሴት አለም ብዙ ታደክመናለች ... ውበታችን ላይ ኢንቨስትመንት ግድ ነው!" ብስራት ገመቹ //በቅዳሜን ከሰዓት//
▶︎

//የሻይ ሰአት// "እንደ ሴት አለም ብዙ ታደክመናለች ... ውበታችን ላይ ኢንቨስትመንት ግድ ነው!" ብስራት ገመቹ //በቅዳሜን ከሰዓት//

ALIKIBA ATEMA NYONGO, HARMONIZE KUWACHUKUA WASANII WAKE AMPA MAKAVU LIVE
▶︎

ALIKIBA ATEMA NYONGO, HARMONIZE KUWACHUKUA WASANII WAKE AMPA MAKAVU LIVE

“MY WIFE TOLD ME I’M NOT THE BIOLOGICAL FATHER OF OUR FOUR CHILDREN”    MR LATEEF
▶︎

“MY WIFE TOLD ME I’M NOT THE BIOLOGICAL FATHER OF OUR FOUR CHILDREN” MR LATEEF

NDOA YA JASINTA MAKWABE ILIVYOYEYUKA WIKI MOJA KABLA YA HARUSI, AFUNGUKA A - Z!
▶︎

NDOA YA JASINTA MAKWABE ILIVYOYEYUKA WIKI MOJA KABLA YA HARUSI, AFUNGUKA A - Z!

HARMONIZE AFUNGUKA KUTUMIKA NA WCB UGOMVI WA RUGE MUTAHABA NA DIAMOND , AANIKA KILA KITU
▶︎

HARMONIZE AFUNGUKA KUTUMIKA NA WCB UGOMVI WA RUGE MUTAHABA NA DIAMOND , AANIKA KILA KITU

WOLPER AFUNGUKA SABABU ZA DIAMOND KUMUIMBIA WIMBO WA MAWAZO / SIJUI KAMA NILIMUUMIZA
▶︎

WOLPER AFUNGUKA SABABU ZA DIAMOND KUMUIMBIA WIMBO WA MAWAZO / SIJUI KAMA NILIMUUMIZA

MBUNGE SHIGONGO AMLIZA MAMA ALIYEMWAMBIA AENDE BENKI AKACHUKUE PESA - ASEMA ALIDHANI UTANI...
▶︎

MBUNGE SHIGONGO AMLIZA MAMA ALIYEMWAMBIA AENDE BENKI AKACHUKUE PESA - ASEMA ALIDHANI UTANI...

YOURS BEFORE WORDS - MAURICE SAM, PEARL WATS, Latest 2026 Nigerian Movie
▶︎

YOURS BEFORE WORDS - MAURICE SAM, PEARL WATS, Latest 2026 Nigerian Movie

MTAFARUKU: Wazanzibari Wawachonokoa Watanganyika
▶︎

MTAFARUKU: Wazanzibari Wawachonokoa Watanganyika

MZEE YUSUPH - Mke Kufariki / Kuacha & Kurudi Kwenye Muziki / Ugomvi na Amigo / ASIMULIA YOTE
▶︎

MZEE YUSUPH - Mke Kufariki / Kuacha & Kurudi Kwenye Muziki / Ugomvi na Amigo / ASIMULIA YOTE

BURNT PRIDE - MAURICE SAM, REGINA DANIELS, OCHANYA, MAUREEN IHUA latest 2026 nigerian movie
▶︎

BURNT PRIDE - MAURICE SAM, REGINA DANIELS, OCHANYA, MAUREEN IHUA latest 2026 nigerian movie

Fally Ipupa - Wanna Dance (Clip Officiel)
▶︎

Fally Ipupa - Wanna Dance (Clip Officiel)

MAPYA YAIBUKA MAMA LOVE KUNGWI AMCHANA DIVA AMEKOSEA KUTAJA MAREHEMU ANGEOMBAMSAMAHA MAREHEMU ASEMWI
▶︎

MAPYA YAIBUKA MAMA LOVE KUNGWI AMCHANA DIVA AMEKOSEA KUTAJA MAREHEMU ANGEOMBAMSAMAHA MAREHEMU ASEMWI

MZEE GEORGE: ATHIBITISHA RASMI UWANJA KUJENGWA VIFAA KUTOKA CHINA VIMELETWA
▶︎

MZEE GEORGE: ATHIBITISHA RASMI UWANJA KUJENGWA VIFAA KUTOKA CHINA VIMELETWA

SALHA ABDALAH ageuka mbogo tetesi za CHANUO kutembea na DR MACHUPA
▶︎

SALHA ABDALAH ageuka mbogo tetesi za CHANUO kutembea na DR MACHUPA

PHINA AONESHA PETE, AFUNGUKA SAFARI YAKE YA MAPENZI NA ENI, MUZIKI & FASHION
▶︎

PHINA AONESHA PETE, AFUNGUKA SAFARI YAKE YA MAPENZI NA ENI, MUZIKI & FASHION

JUMA LOKOLE AFUNGUKA BIFU LA MASHA LOVE NA GIGY MONEY/HAWAPENDANI KWELI/RUSHYANA NA NDARO NI WAPENZI
▶︎

JUMA LOKOLE AFUNGUKA BIFU LA MASHA LOVE NA GIGY MONEY/HAWAPENDANI KWELI/RUSHYANA NA NDARO NI WAPENZI

LEMA AONGEZEWE ULINZI ATOBOA SIRI NZITO YA YUDA ANAEZUNGUMZIWA, "MBUNGE KATUMWA", MOTO WAWAKA
▶︎

LEMA AONGEZEWE ULINZI ATOBOA SIRI NZITO YA YUDA ANAEZUNGUMZIWA, "MBUNGE KATUMWA", MOTO WAWAKA