Kupata kuona kwa Bartimayo Marko 10:46-52

Mpangilio; 10:46a Mukthada 10:46b-47 Bartimayo anaomba msaada 10:48a Watu wanajaribu kumkemea 10:48b-50 Yesu anawaambia wamlete 10:51-52 Yesu anamponya Yesu anamponya kipofu Bartimayo (Mat 20:29-34; Luka 18:35-43) 46Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu, mwana wa Timayo aitwaye Bartimayo, alikuwa ameketi kando ya barabara, anaomba maskini. 47Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!” 48Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!” 49Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.” 50Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu. 51Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.” 52Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani. 46a Mukhtada Katika safari zake amefika Yeriko na wakati anapoondoka wanapita karibu na jamaa ambaye ni kipofu. 46b-47 Batimayo anaomba ahurumiwe Bartimayo anaita ”Yesu Mwana wa Daudi” ni maneno kama hayo yanayoweza kumhatarisha Yesu kwa sababu Daudi alikuwa kiongozi wa kijeshi na hiyo inaweza ikaeleweka vibaya sana kwa wanao tawala. Lakini jamaa aachi hata wakati watu wanajaribu kumkemea 48a Anakemewa na watu Wanapojaribu kumkemea, anaongeza sauti na anaita YESU MWANA WA DAUDI NIHURUMIE!! 48b-50 Yesu anamuita Anapoitwa Bartomayo anatimuka kwa mbio, alitupa vazi lake na kumkimbilia Yesu. Kumbuka ni kipofu! Bila shaka vazi lake lilikuwa vazi la kuonyesha kua yeye ni mlemavu. 51-52 Yesu anamponya Anapomfikia Yesu, anapata swali, unataka nini? Utafikiri Yesu hajui, na labda utaona kama vile anamchokoza kabisa kwa kuuliza swali iliyo wazi kabisa jibu lake Lakini tumekuja kujifunza kwamba ni muhimu kutamka hitaji letu kwa Mungu, ni hatua ya imani. Bartimayo hana shida kujibu swali anasema ”niruhusu nione tena” na Yesu anaruhusu Bartimayo anaona hapo hapo! Tunajifunza nini? Tumepata kuhadisiwa mara nyingi sasa juu ya uponyaji na kuna mambo yanayojitokeza sana Watu wanaomba msaada, wenyewe au kwa kupitia mtu anaowajua Mara nyingi Yesu anapenda watamke hitaji lao Uweza wa Mungu wa kuponya si wa kushakia, ni wa uhakika. Yesu yuko tayari kuwasikiliza watu wote.