SALA YA IMANI// VOICE OF PRAISE CHORALE// OFFICIAL VIDEO

Mchana Jua Lachoma, Usiku NI Homa, Na Pesa Hakuna. Tumbo Linauma, Nyumbani Huruma, Chakula hakuna. Mama Analia Baba Analia . Watoto Wanalia Wamefukuzwa Shule Maana Hata Karo Hakuna.*2 Tukimbilie Wapi, tumgeukie Nani ? Tunapepesa Macho Kuona kwamba kumbe Ukoo Hawatutaki tena*2 Siwezi Kwenda Popote Tetete Nimeshazunguka Kote Tetete Usiku Na mchana pameshashindikana Nakaribia Kukata Tamaa. Akisema Subiri, Subiri. Hapana, Usilazimishe. Ndiyo, Nawe Pokea Kwa Ahsante. Yeye ajua Magumu Kwetu. Lakini Zaidi Ya Yote, Ndugu Zangu Msiape. Wala Kwa Mbingu wala Kwa nchi Wala Kwa Kiapo kingine Chochote. Amepatikana na mabaya? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi. Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Uwezo wote ni kwa Yesu. Saa Ya sala walochoka Sana, Miguuni pake watapata Raha.